Picha
juu na chini ni Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari
(Singpress) mkoa wa Singida wakijifunza uandishi wa habari kupitia
mtandao. Mafunzo hayo ya siku nne yamefanyikia katika ukumbi wa mikutano
wa ofisi ya mkuu wa wilaya Iramba. Mwenye fulana ya misitari ni
mkufunzi wa mafunzo hayo ya uandishi kupitia mtandao (on line
journalism),John Mnubi akiwaelekeza wanachama wa Singpress namna ya
kufungua blog.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Kiomboi
Wanachama
wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida,
wametahadharishwa na vitendo vya ngono zembe vinavyochochea maambukizi
mapya ya virusi Ukimwi kwa madai kwamba baadhi ya wanawake wa mjini
Kiomboi Wilaya ya Iramba hawajui kusema ‘hapana’ pindi wanapoombwa kuwa
na mahusiano ya kimapenzi.
Mwenyekiti
wa Singpress,Seif Takaza ambaye ni mkazi wa mjini New Kiomboi,ametoa
tahadhari hiyo wakati akiwakaribisha wanachama 15 wa Singpress
wanaohudhuria mafunzo ya siku nne ya uandishi bora wa habari kupitia
mtandao (on line Journalism).
Mafunzo
hayo yanayosimamiwa na Mwezeshaji John Mnubi kutoka mkoa wa
Iringa,yanaendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
ya Iramba mkoani Singida.
Akifafanua,Takaza
alisema baadhi ya wanawake na wasichana wa mjini hapa,wana tabia ya
kuchangamkia wageni hususani wanaokuja kuhudhuria mikutano na semina
mbalimbali kwa madai kwamba wanakuwa na fedha za kutosha.
“Mimi
niwatahadharishe tu wanachama wenzangu kwamba muwe waaangalifu na wala
msiponzwe na upatikanaji rahisi wa akina ‘dada poa’ hao.Tambueni kwamba
UKIMWI upo na bado hauna chanjo wala tiba hadi dakika hii”,alisema
Takaza.
Kwa
upande wake Mwezeshaji Mnubi,ameishauri serikali kuhakikisha mkogo wa
mawasiliano taifa unapatikana katika sehemu zote za nchi,ili kusaidia
kupatikana kwa urahisi mitando ya intaneti.
“Kwa
sasa sehemu nyingi nchini hazina huduma ya mitandao ya intaneti na kama
ipo,inapatikana kwa shida kubwa.Mitandao hiyo ikipatikana kupitia
mitandao ya intaneti, itasaidia wananchi wakiwemo wakulima kupata
taarifa mbalimbali pamoja na kujielimisha kwa ajili ya maendeleo
yao”,alisema Mnubi.
Baadhi
ya wanachama wa Singpress,wamedai kuwa pamoja na kupata mafunzo juu ya
matumizi ya mitandao katika kutoa taarifa mbalimbali,elimu hiyo
waliyopata haitawasaidia katika majukumu yao kwa madai kuwa huduma ya
intaneti ni shida kupatikana.
Post a Comment