Kamishna
wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza, Deonice Chamulesile
akiwaongoza Mamia ya Waombolezaji katika kutoa heshima za mwisho kwa
Marehemu Sajini wa Magereza, Peter Shelukindo aliyefariki kwa ajali ya
gari Aprili 22, 2014 majira ya saa Saba mchana wakati akisindikiza
Mahabusu kutoka Mahakama ya Mwanzo Kimanzichana Wilayani Mkuranga, Mkoa
wa Pwani. Katika ajali hiyo pia walikufa Mahabusu wanne waliokuwa
wanatoka kusikiliza kesi zao.
Baadhi
ya Askari wa Jeshi la Magereza wakiaga mwili wa Marehemu Sajini wa
Magereza, Peter Shelukindo katika Kambi ya Chuo cha Maafisa Magereza
Ukonga, Jijini Dar es Salaam leo Aprili 24, 2014.
Mke
wa Marehemu Sajini wa Magereza, Peter Shelukindo akisaidiwa na mmoja wa
Waombolezaji kumuaga Mme wake aliyefariki kwa ajali ya gari.
Mmoja
wa ndugu wa Marehemu akiwa amebebwa na Waombolezaji baada ya kuzimia
katika tukio la kuaga mwili wa Marehemu Sajini wa Magereza Peter
Shelukindo.
Baadhi
ya Waombolezaji walijitokeza kuuaga mwili wa Marehemu Sajini wa
Magereza Peter Shelukindo aliyekufa kwa ajali ya gari Wilayani
Mkuranga(wa kwanza kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa
Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Post a Comment