Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TASAF na washirika wa maendeleo wanaofadhili Mpango wa kunusuru Kaya Masikini na zinazoishi katika mazingira hatarishi watembelea kisiwani Zanzibar


 Mkuu wa Mkoa wa Kusimni Unguja.Dkt. Idris Muslim Hijja, akizungumza na Ujumbe wa Tasaf  na Wawakilishi wa kutoka Nchi Wafadhi wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini PSSN  kabla ya kutembelea Shehia ya Kikungwi.
  Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF mwenye suti nyeusi Ndg. Ladisilaus Mwamanga, akizungumza katika  Ofisi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dkt Idris Muslim Hijja, kabla ya kuaza kwa ziara hiyo.
 Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia Bi. Ida Manjoro, akizungumza wakati walipofika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja kujitambulisha kwake kabla ya kuanza kwa ziara yao kutembelea Kaya Masikini Unguja.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ndg. Ladisilaus Mwamanga, akizungumza na Walengwa wa Kaya Maskini katika shehia ya Kikungwi Unguja. 
 Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini  katika shehia ya Kikungwi Wilaya yaKati Unguja wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf akizungumza katika mkutano huo.

 Picha ya pamoja

=======  =====  =======
Ujumbe kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF na washirika wa maendeleo wanaofadhili Mpango wa kunusuru Kaya Masikini na zinazoishi katika mazingira hatarishi uko kisiwani Zanzibar kuona namna Mpango huo unavyotekelezwa kisiwani humo. Ujumbe huo umepata fursa ya kutembelea shehia ya Kijini Matemwe mkoa wa Kaskazini Unguja na Shehia ya Kikungwi wilaya ya Kati mkoa wa Kusini Unguja ambako umezungumza na walengwa wa  mpango huo.

Wakizungumza na viongozi hao baadhi ya walengwa wameonyesha kuridhika na mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo wamesema maisha ya kaya hizo yameanza kuboreshwa huku mmoja wa walimu wa shule ya msingi Kikungwi Amrani Kombo akibainisha kuwa tangu kuanza kwa Mpango huo  mwaka jana kumekuwa na mahudhurio mazuri kwa wanafunzi kutoka katika kaya masikini ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kabla ya kuanza kwa mpango huo.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga amesema Mpango huo umeanza kutekelezwa kwa awamu nchini baada ya serikali kuridhia utekelezaji wake katika jitihada za kupambana na umasikini miongoni mwa wananchi. Amesema  utafiti umefanywa kwa kina kuona namna ya kuutekeleza mpango huo ili uweze kuleta mabadiliko chanya katika ya maisha  ya wananchi wanajumuishwa katika mpango huo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top