Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WATANZANIA KUTOYUMBISHWA NA WASIOITAKIA MEMA NCHI YAO



Frank Mvungi-Maelezo


KAMATI  ya Tanzania Kwanza nje ya Bunge la Katiba imewataka Watanzania kutoyumbishwa na misimamo ya watu wachache wasioitakia mema Tanzania.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo  Augustino Matefu wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.

Matefu alisema kamati hiyo imeona ni vyema ikawahamasisha Watanzania kuungana na kuwa na mshikamano katika kipindi hiki cha mchakato wa Katiba mpya ili Taifa liwezekuwa na ustawi.

“Sisi kama vijana wazalendo tumeweka Utaifa kwanza vyama baadae  ili kuwahamasisha vijana kote nchini kushikamana na kulinda Tunu za Taifa letu na kupinga kwa dhati  wale wote wanaotaka kwenda kinyume na misingi madhubuti iliyowekwa na waasisi wa Taifa Letu”, alisema Matefu.


Alieleza kuwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa wanaweka maslahi ya Taifa kwanza na vyama vyao baadae ili Malengo ya mchakato wa Katiba mpya yaweze kufikiwa.

Naye Mjumbe wa Kamati hiyo, Renatus Muabi alisema kuwa ni vyema Watanzania wote wakaungana katika kipindi hiki cha mchakato wa katiba mpya  na kufanya kila jambo kwa kuzingatia umuhimu wa Katiba mpya na kuacha itikadi za vyama vyao ili kutoa kipaumbele kwa mambo yenye maslahi kwa Taifa.
Kamati ya Tanzania Kwanza nje ya Bunge  imeandaa maandano ya amani na Mikutano ya hadhara kikanda katika kanda  ya Kaskazini,Nyanda za Juu Kusini,Kanda ya Magharibi,Kanda ya Kati.

Maandamano na mikutano hiyo itafanyika pia katika Kanda ya Kusini,Kanda ya Mashariki,Kanda ya Mwanza,Zanzibar na Unguja huku lengo likiwa ni Kuhamasisha umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania katika kipindi hichi cha mchakato wa Katiba mpya.



Kamati ya Tanzania Kwanza nje ya Bunge la Katiba imeundwa na wajumbe toka vyama 7 vya siasa hapa nchini wakiwa na lengo moja la kuhamasisha
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top