MTANGAZAJI wa
Clouds Redio na TV, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’, juzikati alijikuta
akitwangana makonde na mrembo mmoja ambaye jina lake halikuweza
kufahamika mara moja baada ya kupishana kauli kwenye ukumbi mmoja wa
starehe pande za Kahama, Shinyanga.
Katika tukio hilo, Fetty aliyekuwa
kwenye ‘tour’ ya Serengeti Fiesta alizama ukumbini hapo usiku na baada
ya muda mfupi paparazi wetu alishangaa kumuona akizichapa na mrembo huyo
ikidaiwa walizinguana, hata hivyo waliamuliwa kabla mambo hayajawa
mabayaw.
Ziara ya Tamasha la Fiesta kesho itahamia Tanga ambapo wasanii kibao wataangusha burudani ndani ya Uwanja wa Mkwakwani.
Post a Comment