Stori: Musa Mateja, Kahama
MTANGAZAJI wa
Clouds FM, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty’ na DJ Muli B, wamenaswa wakiwa
kwenye pozi la mahaba huku tena wakiwa wamejisahau utadhani mume na
mkewe.
Mtangazaji wa Clouds FM, Fatuma Hassan ‘DJ Fetty' akiwa na 'DJ Muli B’.
Ishu
hiyo ilitokea Agosti 17, Mwaka huu ndani ya Uwanja wa Kahama, ambapo
walienda kwa ajili ya kutazama burudani za Serengeti Fiesta 2014
zilizokuwa zikifanyika siku hiyo.
Wakiwa
nyuma ya jukwaa, wawili hao walionekana kubebana wakati wamekaa jambo
lililowafanya baadhi ya wasanii waliokuwa nyuma yao kukonyezana na
wengine kuulizana maswali ambayo hayakuwa na majibu kama ni wapenzi au
laa.
‘DJ Fetty' na 'DJ Muli B’ wakila ujana.
Paparazi
wetu apowauliza kama wana uhusiano wowote, wawili hao walikanusha na
kusema wamepozi kama mtu na mfanyakazi mwenzake Clouds FM.
Post a Comment