Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LAANA YA KANUMBA YAIMALIZA BONGO MUVI


IMEVUJA! Kuvunjika kwa Kundi la Bongo Movie Unity kumedaiwa kuwa ni laana ya aliyekuwa memba hai wa kundi hilo, marehemu Steven Kanumba kutokana na kumnyanyapaa enzi za uhai wake, Ijumaa linakupa mchapo kamili.
Marehemu Kanumba.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kanumba alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa kundi hilo lakini kabla hajafa, yaliibuka majungu ambayo yalimsababisha ajiengue na kususia kundi hilo huku akiwa na kinyongo moyoni.

Wakilia juu ya kaburi la marehemu Kanumba.

“Kanumba hakufurahishwa na majungu yaliyokuwa yakiendelea ndani ya klabu dhidi yake, akajiapiza kwamba hatakaa akashiriki masuala ya kundi hilo hadi pale wahusika watakapojisafisha.
“Wakati sisi tukipanga yetu, Mungu naye anapanga yake. Kanumba alifariki wakati ambao wasanii waliomsukia majungu hayo hawajajisafisha, kama si kumuomba msamaha,” kilisema chanzo.

Staa wa filamu Bongo, Jackline Wolper.

KATIBU ASAKWA
Baada ya kunyaka maelezo hayo ya chanzo chetu, mapaparazi wetu walianza kuwatafuta waliokuwa viongozi wa klabu hiyo na kufanikiwa kumpata aliyekuwa katibu msaidizi, Devotha Mbaga, ambaye alikiri kwamba klabu hiyo ina laana ya Kanumba.

HUYU HAPA DEVOTHA
Akizungumza kwa hisia kali maeneo ya nyumbani kwake Kigamboni, jijini Dar, Devotha alisema mgogoro unaoendelea ndani ya kundi hilo ambalo linapumulia mashine baada mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na katibu wake, William Mtitu kujiuzulu ni laana ya Kanumba hivyo wanatakiwa kuomba radhi kaburini kwake.


Alisema enzi za uhai wa Kanumba baadhi ya wasanii ambao wanagombana chini kwa chini kwa sasa ndani ya kundi hilo (majina yapo), walimnyanyapaa na walikuwa wakimchukia na kufikia hatua ya kuwakataza wanachama wote kutoshiriki kwenye filamu zake.

“Ukweli baadhi ya wasanii hasa hao viongozi wanatakiwa kutambua makosa waliyomfanyia Kanumba enzi za uhai wake na wamuomba msamaha kwani walimkosea sana na wakishaomba, naamini Bongo Movie itasimama lakini wasipofanya hivyo hiyo laana itaendelea kuwatesa na watapigana kila siku.

“Yaani kuna wakati hadi huwa nafikia hatua ya kusema bora Kanumba alikufa mapema yawezekana Mungu alikuwa na kusudi lake maana angeaibika na angeonekana ni mtu asiyefaa katika jamii kutokana na mikakati ambayo wasanii wenzake walikuwa wameipanga,” alisema Devotha.

Aliyekuwa mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Stive Mengere.

KUMBE WALIWAHI KUKAA KIKAO
Kama hiyo haitoshi, katika aya nyingine, Devotha alisema kuna wakati waliwahi kuweka kikao cha kusameheana kilichoandaliwa na Ridhiwan Kikwete ambaye sasa ni Mbunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) lakini mambo bado yakawa ‘shagala baghala’.

“Nakumbuka kwenye kikao kimoja ambacho aliitisha Ridhiwan Kikwete kwa ajili ya wasanii na kusema kama kuna mtu amemkosea mwenzake wasameheane baada ya kuongea na sisi na kuondoka, watu walianza kuongea maneno mabaya ya kashfa na hapo ndipo walipopanga mikakati ya kumchafua na kutofanya kazi na Kanumba lakini baada ya siku chache alifariki.

Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'.
 
“Hao wanaogombana sasa hivi ndiyo walikuwa vinara katika kumnyanyapaa Kanumba na ndiyo haohao siku ya mazishi yake ndiyo waliobeba jeneza, msalaba na kuvaa suti wakati walikuwa hawako naye vizuri, unajua roho huwa haifi kwa hiyo wanatakiwa kuomba msamaha ili wawe na amani,” alisema Devotha.
NI LAANA NZITO?
Kwenye mazungumzo hayo na waandishi wetu, Devotha aliendelea kutiririka kuwa kutokana Kanumba kufariki dunia akiwa na kitu moyoni kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna kitu alikizungumza muda mchache kabla hajafariki au kuwa na kinyongo na Bongo Movie hivyo wasanii hao wanatakiwa kwenda kuomba msamaha kaburini kwake ili kundi hilo lisimame tena.

Staa katika tasnia ya filamu Bongo Dk. Cheni.

WAOMBA RADHI KIMYAKIMYA
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba kuna baadhi ya wasanii wamedaiwa kuanza kwenda kaburini hapo kimyakimya na kuomba radhi ili kundi lao lirudi kwenye mstari kama lilivyokuwa enzi za marehemu Kanumba.

“Tumeona hali ni mbaya bora twende vinginevyo mambo yataharibika zaidi ya hapa,” alisema msanii mwenye taito kubwa ndani ya Bongo Movie kwa sharti la kustiriwa jina.


WENGINE KUOMBA RADHI
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya wasanii kwa sharti la kutotaja majina yao ambao walikiri kwamba mambo hayaendi sawa kutokana na laana ya Kanumba hivyo wako mbioni kwenda kuomba msamaha katika kaburi lake wakiamini uliokufa ni mwili roho ingali hai.


KUMBUKUMBU
Marehemu Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza-Vatcan akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael ‘Lulu’. Alizikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar. 


>>>GPL
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top