Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Bw. Nape Nnauye, amewataka wananchi wasikubali kuandamana kwa shinikizo la viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ili kushinikiza Bunge Maalumu la Katiba lisitishe vikao vyake kabla ya Oktoba 4,2014.
Bw.
Nnauye aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Wilaya
ya Kisarawe, mkoani Pwani na kusisitiza kuwa, maandamano hayo aachiwe
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bw. Freeman Mbowe, familia yake na viongozi
wengine.
Alisema
chama hicho kina utamaduni wa kutumia damu za Watanzania kama mtaji
wake kisiasa kwani vyombo vya dola vinapochukua hatua ya kuzuia
maandamano, wanaoathirika si viongozi wa chama hicho au familia zao ndio
maana wanaona fahari watu wanapokufa.
"Upinzani
katika nchi hii umegeuka kuwa laana, kazi kubwa ambayo wanaifanya ni
kuchonganisha watu na Watanzania ni mashahidi, maeneo ambayo CHADEMA
wamefanya maandamano, watu maskini wamepoteza maisha.
"Viongozi
wa CHADEMA wanabaki salama na familia zao hivyo kama Mbowe anataka
kufanya maandamano nchi nzima kushinikiza Bunge la Katiba lisitishwe, aanze kutangulia yeye, mkewe na watoto wake, Watanzania wamechoka kushuhudia damu za watu maskini zikimwagika," alisema Nape.
Aliwataka
wananchi kufahamu kuwa, Katiba haimpeleki mwanasiasa au mtu yoyote
Ikulu badala yake kura ndizo zinazoweza kumpeleka Ikulu ambapo CHADEMA,
Chama cha Wananchi (CUF) pamoja na NCCR-Mageuzi, wanaamini Katiba
ikipatikana ndio inayoweza kuwapa ushindi katika Uchaguzi Mkuu 2015.
"Vyama
hivi vinataka kuligawa Taifa kwa kutumia mchakato wa Katiba, umefika
wakati wa Watanzania kuachana na upinzani wenye kujenga chuki...CCM na
viongozi wake wamekuwa wakihubiri amani, mshikamano na umoja lakini
wapinzani wanatumia muda mwingi kuhubiri chuki," alisema.
Katika
hatua nyingine, Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Abdulrahman Kinana, amepongeza
juhudi za Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama
Salma Kikwete, kwa juhudi zake za kuwasaidia wanawake na watoto wa kike
kupitia taasisi hiyo.
Bw.
Kinana alitoa pongezi hizo juzi baada ya kutembelea Shule ya Wanawake
ya Wama Nakayama, inayomilikiwa na taasisi hiyo iliyopo kwenye Kijiji
cha Nyamisati, Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani.
Alisema
Mama Kikwete amekuwa na mchango mkubwa nchini kutokana na jitihada zake
za kusaidia makundi mbalimbali wakiwemo watoto yatima na waishio katika
mazingira magumu.
Aliwataka
wanafunzi shuleni hapo, kusoma kwa bidii ili kuunga mkono juhudi za
Mama Kikwete kwani wao ndio viongozi wa baadaye ambao watashika nafasi
mbalimbali za uongozi.
Kwa
upande wake, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Suma Mensah, alisema shule
hiyo imekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Rufiji na nje ya Wilaya hiyo
kwani inatoa elimu kwa wanafunzi wasio na uwezo pamoja na yatima.
"Juhudi
za Mama Kikwete kwa watoto wa kike zimefanikiwa kwani watoto waliokuwa
hawana mwelekeo wa maisha, hivi sasa wanafurahia kupata elimu bora," alisema Mensah.
Post a Comment