Mwenyekiti
wa Umoja wa Vijana Wazalendo wa Vyuo vya Elimu ya Juu Mkoa wa Dar es
Salaam, Mussa Omary (katikati), akizungumza na waandishi wa habari
wakati akisoma tamko hilo. Kulia ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (UDSM), Theodora Malata na Mwanachuo Chuo cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere, Rehema Akukweti.
Mwanachuo
wa UDSM, Gulatone Masiga akijibu maswali ya waandishi wa habari.
Kushoto ni Mwanachuo Mwita Nyarukururu na Mwenyekiti wa umoja huo, Mussa
Omary.
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Theodora Malata, akichangia jambo wakati wa kujibu maswali ya wanahabari.
Mwanachuo
Mussa Mashamba kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, akisisitiza jambo
wakati akijibu maswali ya wanahabari. Kulia Massoro Kivuga na William
Haule.
Wawakilishi wa wanafunzi wa vyuo vikuu 12 vya Mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari.
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.Picha na habari za jamii.com-simu namba 0712-727062
*********
TAMKO
RASMI LA UMOJA WA VIJANA WAZALENDO WA VYUO VYA ELIMU YA JUU DAR ES
SALAAM LA KULAANI KAULI ZA MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA ZA KUHAMASISHA
UASI KWA NJIA YA MAANDAMANO
Sisi
ni vijana wasomi wazalendo kutoka vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko Dar
es Salaam, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM); Chuo Kikuu cha Ardhi
(ARU); Dar es Salaam University College of Education (DUCE); USTAWI WA
JAMII; Chuo Kikuu cha Mtakatifu John (St. John); Chuo cha Usimamizi wa
Fedha (IFM); Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT); Kampala International
University (KIU); Dar es Salaam Institute of Technology (DIT); Institute
of Adult Education (IAE); Tanzania School of Journalism (TSJ); College
of Business Education (CBE), Chuo cha Uhasibu (TIA) na Chuo cha
kumbukumbu ya Mwl JK Nyerere.
Tunachukua
fursa hii kulaani vikali kauli zilizotolewa na Mh. Freeman Mbowe ambae
ni Mwenyekiti wa CHADEMA ya kutaka kuitisha maandamano ya nchi nzima
bila kikomo pamoja na kuhamasisha asasi nyingine za kiraia kufanya na
kuratibu maandamano kama hayo ya CHADEMA kwa ajili tu ya kupinga
kuendelea kwa Bunge Maalumu la Katiba.
Tunawaambia
watanzania wenzetu kuwa tumekerwa na kusononeshwa sana na kauli ya
kibabe ya kiongozi huyu wa CHADEMA ya kuhamasisha vurugu ambazo
tumezishuhudia zikisambaratisha umoja wa nchi nyingi na kuwa chanzo cha
vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo huwa haviishi na hatimaye kuendelea
kulipakazia Bara la Afrika kuwa halijastaarabika na siasa za
kidemokrasia.
Tulimsikia
akiahidi maandamano bila kikomo kwa kibali cha polisi au bila kibali
cha polisi mbele ya wajumbe ambao wengine sio watanzania. Ndugu
watanzania wenzetu, kauli kama hii haiwezi kusemwa hata na Rais yeyote
ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu anaeongoza kwa kufuata misingi ya sheria na
utawala bora, je Mh. Mbowe anapata wapi uhalali na ujasiri huo? Maana
Rais na Amiri Jeshi Mkuu ambae ni dikteta anaweza kusema lakini yule
anaetawala kwa misingi ya sheria, katiba na utawala bora kamwe hawezi
kusema kauli kama hizo. Maneno aliyoyasema Mh. Mbowe amejivalisha
madaraka zaidi hata ya yale ya Rais wetu ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa
Vikosi vya Ulinzi na Usalama. Lakini kwa mtazamo wetu ni kuwa Mh. Mbowe
amejivalisha UDIKTETA ambao unatakiwa kulaaniwa na kila mtanzania
aliyeko ndani na nje ya nchi hii. Uzito wa kauli zake haubebeki na mtu
yeyote kwenye taifa hili. Hatuna shaka kuwa ametoa kauli mbaya sana
kuliko zote za kisiasa ambazo zimewahi kusemwa majukwaani.
Watanzania
kwa ujumla wetu na makundi yetu tukikaa kimya bila ya kuzilaani na
kuzikemea vikali kauli zake, tutakuwa hatujitendei haki sisi wenyewe na
pia hatutavitendea haki vizazi vijavyo vya nchi yetu.
Ndugu
zetu watanzania, kama ambavyo yeye mwenyewe alisema kabla ya kutoa amri
kwa watu kuandamana kuwa anaamini watanzania wapo tayari kufanya
mageuzi ili chama chake kingie IKULU ya Magogoni. Hayo yatafanikiwa
endapo tu vijana wataacha uoga, maneno ambayo yanaashiria kutaka
kuchukua uongozi kwa nguvu bila kufuata misingi ya kidemokrasia
inayosimamiwa na serikali iliyo madarakani.
Sisi
umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es Salaam
tunasema kuwa uzito na ubaya wa kauli hizi unaonesha wazi kuwa Mh.
Freeman Mbowe hafai kupewa dhamana ya kuwa Rais wa nchi na Amiri Jeshi
Mkuu wa vikosi vya ulinzi na usalama na pia amedhihirisha kuwa CHADEMA
haina sifa ya kuiongoza nchi hii kwa sasa kwa kufuata misingi ya
demokrasia na kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa watanzania kwa
lengo la kudumisha umoja, na muungano wetu.
Tunaomba watanzania mkumbuke
na mtilie maanani kuwa, Mh. Freeman Mbowe katoa kauli hizi akiwa raia tu
wa kawaida. Je itakuwaje akiwa Rais wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa
Vikosi vyetu vya Ulinzi na Usalama wa nchi hii? Kwa maoni yetu ni kuwa
kwa upeo na mtazamo wa akili yake hakuna atakaebaki salama ndani ya nchi
hii kwa kuwa atatuingiza kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe na pia
atatuingiza kwenye vita na nchi majirani. Hafai, hafai, hafai hata mara
moja kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu. Ndugu watanzaia, hivi ni mtu gani
anaeweza kuishi kwa amani na viongozi kama Mbowe na wenzake wanaotumia
ubabe kwenye maisha ya kawaida ya kila siku? Na hapa ndipo
wanatuthibitishia kuwa Mh. Freeman Mbowe na Kikundi cha viongozi wa
chama chake wote karibu wameshindwa kuzichunga na kuziweka pamoja
familia zao na hatimaye zimesambaratika kwa ubabe huo huo, hivyo
hawataweza kutuongoza na kutuweka pamoja watanzania ili tuishi kwa
amani.
Ndugu
watanzania wenzetu tumebaini kuwa Mh. Freeman Mbowe na viongozi wenzake
wa CHADEMA wanatumia maandamano na damu za watanzania kutafuta fedha
kwa wafadhili wao ambao hawaitakii mema nchi yetu. Wakiaandaa
maandamano, wanapiga picha na kuwapelekea wafadhili wao, wanapata fedha,
wanajenga majumba na kununua magari ya kifahari na kusafiri ulaya,
marekani na familia zisizo rasmi kwa kujificha kwenye pazia la
DEMOKRASIA huku watanzania wakiendelea kuathirika na maandamano. Hapo
ndugu watanzania hakuna DEMOKRASIA bali tunaona DOMO-KRASIA na
BONGO-KRASIA, yaani wanatumia ulimi na akili ndogo za kitoto
kujinufaisha na familia zisizo rasmi kwa siasa za ulaghai, ghilba,
fitina, majungu, choyo, chuki, usanii wa kisiasa na uhaini alioutangaza
Mh. Mbowe.
Ndugu
zetu watanzania, fahamuni kuwa Mh. Freeman Mbowe, Dk. Wilbroad Slaa,
Tundu Lissu, Godless Lema, Mchungaji Peter Msigwa, Hezekiah Wenje na
wengine wana familia. Swali je mmeshawahi kuwaona wake, watoto, na ndugu
zao wa karibu kwenye maandamano yoyote yale waliyowahi kuyaandaa? Siku
zote huwaambia watu wao hao bakini majumbani mtadhurika. Pale damu za
watanzania zinapomwagika kwenye maandamano baadae huwa wanajifungia na
kushangilia ushindi mkubwa wa kuvuna mabilioni ya fedha za kigeni, kwa
kuwa huwa wanapiga picha matukio hayo na kwenda kuonesha wafadhili wao
kwa taswira kwamba demokrasia inanyanyaswa. Wanakinga mabilioni ya fedha
za kigeni wanatia kwenye akaunti zao, wanagawana, na mambo yao yanaenda
sawasawa, huku watanzania wengine wakiwa wana vilio vya kupoteza ndugu
na baba zao, waume, wake, wapenzi/wachumba, na watoto wao na kadhalika.
Swali kwa nini hawaoni umuhimu wa kujali utu, ubinadamu na uhai wa
watanzania wengine?
Sisi umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es Salaam tunapenda kuwahakikishia kuwa thamani ya maisha ya watanzania wote au hata kwa mtanzania mmoja ni kubwa sana kuliko hiyo katiba mpya wanayoidai.
Tunawaomba
watanzania wenzetu msikubali kufanywa kama mbuzi wa kafara na watu
wenye tamaa, pupa, ulevi, na uroho wa madaraka kama hawa akina Mbowe na
kundi lake. Tusijiendee tu kama kuku aliekatwa kichwa halafu akaachiwa
atembee, na tusishikiwe akili zetu kama za mbayuwayu kwani “Akili za
Kushikiwa, ongeza na zako”. Tuwakataeni wanasiasa uchwara waliofilisika
kihoja na kutaka kuwatumia ili kujinufaisha. Wanataka kutupeleka wapi?
Ni dhambi isiyosameheka kulitumbukiza taifa hili katika machafuko yenye
majuto makubwa kama ya Misri, Syria, Afrika ya kati, Libya, Sudan ya
Kusini na kwingineko. Tusikubali watupeleke huko, waacheni waende
wenyewe kama wanaweza. kwani nchi yetu ina mgogoro wa kisiasa?!!!!!
Waulizeni wanataka nini?
Ndugu
watanzania wenzetu, tunaomba mjue kwenye nchi hizo hizo zenye
demokrasia pevu watu wa aina ya Mh. Freeman Mbowe (hasa kwa kauli zake
alizozitoa juzi tarehe 14.09.2014) wanaotaka kuvuruga na kuvunja misingi
mikuu ya utaifa wao (core values) kama vile amani, usalama na umoja
huwa hawavumiliwi hata kidogo.
Sisi
umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es Salaam
tunaviomba vyombo vyetu vya dola visizivumilie kauli kama hizi
zilizotolewa na Mh. Freeman Mbowe hata mara moja. Kwani vyombo vya dola
vina dhamana ya kulinda, kutunza na kuendeleza amani na utulivu wa nchi
yetu. Umoja wetu, kwa heshima na taadhima kubwa, tunaviomba vyombo hivi
kumchukulia hatua kali za kisheria Mh. Mbowe kwa kauli hii ya kutishia
uvunjifu wa amani kabla hajaiingiza nchi yetu kwenye machafuko ya
kisiasa.
Sisi
umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es Salaam
hatutaki kuona vijana wenzetu na watanzania wote kwa ujumla wakiathirika
kwa ujinga huo wa maandamano yanayofanywa mradi wa kutafuta fedha.
Kwani maandamano hayo yatawaathiri wana vyuo wa Dar es Salaam pamoja na
kuathiri shughuli nyingine za kiuchumi, na kijamii za wananchi wa
kawaida. Kwa nini shughuli zetu na za wananchi zisimame kwa sababu tu ya
machafuko ili Mh. Mbowe apate picha za kwenda kuuza huko kwa wafadhili
wao? Sisi umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es
Salaam tulisikiliza na kutazama hotuba ile kwa umakini wa hali ya juu,
tunapenda kuwathibitishia kuwa hotuba ile haikuwa ya kisomi, ilikuwa
haijengi chama chake wala ilikuwa haijengi nchi yetu isipokuwa ilikuwa
ya kibabe, ilikuwa ya kejeli, ilikuwa ya kichochezi iliyolenga kuvunja
misingi ya amani na utulivu wa nchi yetu. Ni matumaini yetu kuwa hata
kwa mwanafunzi wa shule ya msingi hawezi kujifunza kitu chochote cha
maana kutoka kwenye hotuba ile. Hotuba ya Mh. Mbowe haiwezi kutusaidia
kujenga taifa lenye dira kwa vizazi vijavyo.
Mwisho,
Sisi kama umoja wa vijana wazalendo wa vyuo vya elimu ya juu Dar es
Salaam, tunawataka watanzania wenzetu mzipime na kuzitafakari kwa makini
kauli za Mh. Mbowe, na kujiuliza je anafaa kuwa kiongozi wa nchi hii?
Asanteni kwa kutusikiliza,
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
Imesomwa na Mussa Omari,
Imesomwa na Mussa Omari,
Mwanafunzi OUT,
kwa niaba ya umoja wa vijana wazalendo wa Vyuo vya elimu ya juu
Dar es Salaam
Tarehe 17.09.2014
Tarehe 17.09.2014
Sahihi
……………………….
Simu 0715632681
Post a Comment