JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA
MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
MAADHIMISHO YA SIKU YA UTALII 2014
Wizara
ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana
na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha pamoja na Wadau wa Sekta ya Utalii nchini
wanayofuraha ya kuwakaribisha Wananchi
wote na Wadau mbalimbali katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii
Duniani kwa mwaka 2014 ambayo
Kitaifa yatafanyika Mkoani Arusha
kwenye viwanja vya Nane Nane (TASO) kuanzia
tarehe 20 hadi 28 Septemba, 2014.
Siku
ya Utalii Duniani huadhimishwa tarehe 27 Septemba ya kila mwaka ambapo kila
nchi mwanachama wa Shirika la Utalii Duniani (UNWTO) husherekea siku hii,
kwa lengo la kuweka uelewa kwa Jamii kuhusu umuhimu wa utalii na thamani yake,
kijamii, kisiasa, kitamaduni na kiuchumi.
Kauli
Mbiu ya Mwaka huu ni “Utalii na Maendeleo ya Jamii’’ (Tourism and Community
Development) kwa kuzingatia Kauli Mbiu hii,
tunawajulisha wadau wote katika nyanja mbalimbali za Utalii, Maliasili
na Uhifadhi, vikundi vya jamii na wajasiriamali, viongozi na wataalamu kwa
pamoja kushiriki kikamilifu katika
Maadhimisho ya Siku ya Utalii
Duniani kwa nia ya kujifunza na kutambua fursa za kiuchumi zilizopo katika
Sekta ya Utalii na kutumia fursa hizo kujikomboa katika umaskini.
Shughuli
zitakazofanyika ni pamoja na kuwasilisha na kuonesha na kwa vitendo juu ya
tafsiri ya Kauli Mbiu kwa kufanya kongamano la
ushirikishwaji wa jamii kwenye sekta ya Utalii kwa ajili ya kujiletea
maendeleo, mashindano ya Uchoraji wa picha kuhusiana na kauli mbiu, michezo na
burudani mbalimbali.
Vilevile
kutakuwa na maonesho ya utalii, malikale, misitu na masuala ya uhifadhi kwa
ujumla na bila kusahau ziara ya kutembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
na Hifadhi ya Taifa ya Arusha kwa nia ya kuhamasisha wananchi kushiriki
kwenye shughuli za utalii wa ndani.
Wito
unatolewa kwa kuwaalika wadau wote wa utalii na jamii husika kuja kwa pamoja na
kuadhimisha siku hii kama ishara ya jitihada za pamoja za kufanya utalii nguzo
ya kweli ya maendeleo ya Jamii nchini.
Imetolewa na:
Katibu
Mkuu
Wizara
ya Maliasili na Utalii.
Post a Comment