Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

GARI AINA YA TOYOTA PRADO LAUA MWANAFUNZI

Mwanafunzi mmoja wa darasa la pili katika shule ya msingi Nyamikoma wilayani Butiama mkoani Mara amefariki dunia na watu wengine watatu kujeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na gari moja aina Toyota Prado yenye namba za usajili T767 dbx kasha kupaa na kuparamia nyumba na mashine ya unga katika eneo hilo la pida wilayani humo.
Ajali hiyo mbya imetokea katika eneo hilo la pida katika barabara kuu ya Mwanza-Sirari wakati gari hilo likitokea jijini Mwanza kwenda Nyamongo wilayani Tarime, ambapo imeelezwa kuwa baada ya kugongwa kwa mwanafunzi huyo Keneth Barnaba dereva wa gari alijitahidi kuwakwepa wanafunzi wengine lakini kutokana na mwendo kasi gari hilo lilimshinda na kupaa juu kisha kuvamia jengo la mashine ya kusagia nafaka na nyumba ya familia moja kijijini hapo.


Wakizungumza wakati wa maandalizi ya mazishi ya mwanafunzi huyo baadhi ya wananchi wa kijiji hicho, wameiomba wakala wa kuhudumia barabara nchini Tanroads mkoa wa Mara kuangalia uwezekano wa kuweka matuta katika eneo hilo ili kuzua ajali hizo za mara kwa mara.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top