MFANYABIASHARA
wa mjini Tarime mkoani Mara, Wilson Weso maarufu Kishimba (34) amekufa
kwa kile alichodaiwa amekunywa sumu nyumbani kwa baba mkwe wake.
Inadaiwa
alifanya hivyo nyumbani kwa baba mkwe, Chacha Sasita ambaye ni mkazi wa
kijiji cha Rebu kata ya Turwa, kutokana na mgogoro na mke aliyemtoroka
na kwenda jijini Mwanza na kumwachia watoto wawili.
“Alifariki dunia kwa kunywa kitu kinachodhaniwa ni sumu,” alisema kamanda.
Kwa
mujibu wa kamanda, baada ya mke wa mfanyabiashara huyo kuondoka,
alichukua watoto alioachiwa na kuwapeleka kwa baba mkwe kabla ya kunywa
sumu.
"Mwili
wa marehemu uligunduliwa muda mchache na wakazi wa kijiji hicho cha
Rebu ambapo askari wetu walifika na kuuchukua mwili huo na kuupeleka
chumba cha maiti katika Hospitali ya Wilaya kwa uchunguzi zaidi,”
alisema Kamanda huyo na kuongeza kwamba polisi inaendelea na uchunguzi.
Post a Comment