Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MSHANGAO MPYA MISS TANZANIA 2014

 


Siku chache baada ya kutwaa Taji la Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu ameibua mshangao wa aina yake kutokana na utata wa umri wake, Ijumaa limesheheni data.
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akionesha cheti mara baada ya kuhitimu masomo.
Utata huo uliibuka saa chache mara baada ya shindano hilo kufanyika Oktoba 10, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar ambapo wadau mbalimbali walianza kuhoji.
UTATA WENYEWE HUU HAPA
Mara baada ya mrembo kutangazwa mshindi, habari za chini kwa chini zilidai kwamba Sitti alijinasibu kuwa ana umri wa miaka 18 na elimu ya (digrii mbili) (masters), mambo ambayo yaliwashtua wengi na kuanza kuhoji uhalali wa umri huo ukilinganisha na kiwango chake cha elimu.
“Mh! Haiwezekani, kama ana miaka kumi na nane atakuwa alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili?” Alihoji mdau mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini.


ELIMU YA BONGO IKOJE?
Kwa mfumo wa elimu nchini ulivyo, mtoto huanza darasa la kwanza akiwa na kati ya miaka mitano hadi saba, jambo ambalo haliingii akilini kwa Sitti kwani hesabu zinakataa hata kwa mtu asiyesomea mahesabu.

Ukiachilia mbali shule ya awali (nursery) ambayo huchukua kati ya miaka miwili hadi mitatu, ukihesabu miaka saba ya elimu ya msingi (primary), miaka minne ya sekondari (ordinary level), miaka miwili ya kidato cha tano na sita (advanced level) na miaka mitatu ya shahada kwanza (bachelor degree), jumla ni miaka 16.
Mlimbwende, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
Pia kuna madai kwamba ametumia mwaka mmoja kusomea shahada ya pili (masters) huku kukiwa na muda ambao kwa kawaida huwa unapotea baada ya kumaliza kidato cha nne kwenda cha tano na baada ya kumaliza kidato cha sita kwenda chuo kikuu.
INA MAANA ALIANZA DARASA LA KWANZA AKIWA NA MIAKA MIWILI?
Kwa mantiki hiyo, kama kweli Sitti ana umri wa miaka 18, basi atakuwa alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili, jambo ambalo ni msamiati mpya kwa jamii ya Kibongo.
Mrembo, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akifurahia jambo na marafiki zake wa mamtoni.
BABA MZAZI ANASEMAJE?
Ili kuondoa utata na tafrani inayoendelea kwenye mitandao ya kijamii hadi kufikia hatua ya watu kutukanana, gazeti hili lilimtafuta baba mzazi wa Sitti ambaye ni Mbunge wa Temeke, Dar kwa leseni ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Abbas Zuberi Mtemvu alipopatikana alifunguka:

“Umri wake ni kama alivyosema mwenyewe siku ile (miaka 18), kama mnataka kujiridhisha nendeni hata huko Miss Tanzania mtaoneshwa passport (hati ya kusafiria) yake…,” alisema mzazi huyo huku akiomba aachwe kwanza ashughulikie wananchi wa jimboni kwake.
Sitti Abbas Zuberi Mtemvu akiwa na baba yake, Mhe. Abbas Zuberi Mtemvu.
TUMUAMINI MZAZI?
Hata kama tukiamini maelezo ya mzazi, maana yake ni kwamba mrembo huyo alianza darasa la kwanza akiwa na miaka miwili, jambo ambalo linazidi kuongeza utata katika sakata hilo.

AKATAA KUHITIMU MASTERS
Alipobanwa zaidi kuhusu taarifa zinazosema kuwa mwanaye amehitimu masters, mzazi huyo alikanusha na kudai kwamba mwanaye amehitimu bachelor degree (shahada).
“Kuhusu masters mnakosea, mwanangu hana masters, ana bachelor, nilimshauri achukue masters lakini akaomba nimuache ashiriki kwanza mashindano ya u-miss ndiyo aje aendelee baadaye,” alisema mheshimiwa huyo.
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu wakati wa kutwaa taji
NI AIBU NYINGINE KWA LUNDENGA?
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, suala la warembo kudanganya umri limekuwa ni sugu hivyo kuleta tafsiri ya aibu kwa muandaaji wa mshindano hayo, Hashim Lundenga akidaiwa kupigwa changa la macho pindi anapowapokea katika mchakato wa awali.
Pasipoti ya kusafiria ya Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
“Hii ni aibu nyingine kwa Lundenga kwani haiwezekani mtu akaingia akasema ana miaka kumi na nane halafu awe na elimu kama hiyo, anashindwaje kulibaini hilo mapema?” Alihoji mdau mkubwa wa urembo nchini akikumbushia kisa cha Wema Isaac Sepetu, Miss Tanzania 2006/07 ambaye naye alidanganya umri akasema ana miaka 18 wakati alikuwa na kumi na saba.
Leseni ya udereva ya Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zuberi Mtemvu.
MSIKIE LUNDENGA SASA
Alipotafutwa Lundenga ili kuzungumzia suala hilo, alijibu kwa kifupi na kukata simu:
“I can’t answer that question (Siwezi kujibu swali hilo)…siwezi.”

SITTI ANASTAHILI KUWA NA UMRI GANI?
Ukiachilia mbali muonekano, baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili walisema kuwa ukifuata utaratibu wa mfumo wa elimu Bongo, Sitti alipaswa angalau awe na umri wa miaka 23, hata kama madai ya kurushwa madarasa ni sahihi.

Muandaaji wa mshindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga akifafanua jambo
Yaani angeanza darasa la kwanza akiwa na miaka saba, angesoma shule ya msingi kwa miaka saba, sekondari miaka minne, kidato cha tano na sita miaka miwili na chuo miaka mitatu, jumla angekuwa na umri wa miaka 23 kwa sasa ambayo ni pungufu ya miaka 25 iliyotajwa kwenye wasifu wake mtandaoni huko nchini Marekani. 

SITTI AMEFIKAJE HAPA?
Data zinaonesha kwamba, baada ya kumaliza kidato cha sita, Sitti alihamia jijini Dalas kwenye Jimbo la Texas, Marekani ambapo mbali na kusomea elimu ya chuo kikuu nchini humo, amewahi kuigiza filamu inayojulikana kwa jina la Lost In Abroad.


CHANZO, GAZETI LA IJUMAA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top