Jolly Tumuhirwe akiwa mahakamani leo.
Jolly Tumuhirwe alipokuwa akimtesa mtoto Arnella.
HAUSIGELI aliyenaswa kwenye video akimtesa
mtoto nchini Uganda, amefikishwa mahakamani leo.Mfanyakazi huyo Jolly
Tumuhirwe ameiambia mahakama kuwa anajutilia kile alichokifanya na
anaomba msamaha.Ameshitakiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella.
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly
atashitakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji, kiogozi wa mashitaka
alimshitaki Jolly kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo.
Bi.Tumuhirwe alikiri makosa yake na
kuomba msamaha. Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani
licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila
malipo.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Jumatano ambapo hakimu anatarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jolly.
Huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola mia nne au adhabu zote mbili.
BBC
Post a Comment