Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHIRIKA LA RELI LIMEPOKEA MABEHEWA 50 YA MIZIGO NA 22 YA ABIRIA .... Waziri Mkuu Mizengo Pinda Apokea Mabehewa Mapya ya TRL Yaliyonunuliwa Kwa Fedha ya Serikali


Serikali imepokea mabehewa 50 ya mizigo na mabehewa 22 ya kisasa ya abiria ikiwa ni sehemu ya mabehewa 274 yanayotawarajiwa kuwasili nchni ili kuboresha huduma za usafiri wa mizigo na abiria hapa Nchni.
 Akizungumza na waandishi wa habari, waziri wa uchukuzi Daktari Harrison Mwakyembe amesema kuingia kwa mabehewa hayo ni ishara ya jitihada za serikali katika kuimarisha huduma ya usafiri wa reli ambapo amesema amesisitiza serikali imetumia zaidi ya bilioni 200 katika kuboresha sekta ya reli nchni.
 
 Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa shirika la reli nchni Bwana Kipalo Kisamvu amesema mabehewa hayo ya abiria ni kwa ajili ya safari katika mikoa ya mwanza  na kigoma, na kusisitiza shirika hilo la Reli kwa kushirikiana na wakala wa usafiri wa majini na nchi kavu wako katika mchakato wa kuanzisha usafiri wa haraka wa abiria ambao utasimama katika vituo vikubwa pekee. (Picha na Ernest Nyambo)
 

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Uchukuzi, Dr. Harrison Mwakyembe wakikagyua moja ya mabehewa mapya ya TRL yaliyonunuliwa  kwa fedha ya serikali wakati alipokwenda  kwenye Bandari ya Dar es salaam Desemba 8, 2014  kupokea mabehewa hayo.  
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozwa na Waziri wa Uchukuzi, Dr. Harrison Mwakyembe (kulia kwake) na Naibu Waziri  wake, Dr. Charles Tizeba (kulia) kukagua baadhi ya mabehewa mapya ya Shirika la Reli  nchini (TRL) yaliyonunuliwa na kwa fedha za serikali wakati alipokwenda kwenye bandari ya Dar es salaam Desemba 8,2014.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top