Rais Jakaya
Kikwete amesema atahakikisha kablaya ya kumaliza muda wake wa uongozi anatimiza
ahadi alizozitoa ili kumpungumzia kazi rais ajaye na kuongeza kama kutakuwa kuna
mambo yamebaki atayakabidhi kwa mrithi wake hivyo wananchi wasiwe na wasi
wasi.
Mh Kikwete
ameyasema hayo alipokuwa akihitimisha mafunzo ya maafisa wa Polisi ambapo
amewagiza kuhakisha kuwa mauaji ya Alibino yanakoma.
Aidha Mh rais
amelitaka jeshi hilo la polisi kuhakisha inajiepusha na vitendo vya rushwa kwani
vinalichafua pamoja na kuongeza nguvu kupambana matukio ya ugadi ambayo kwa sasa
yameanza kushamiri nchini.
Kwa upande wake
naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh Pereira Silima amewataka polisi
kwakuwa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia na hivyo lazima wafanye mambo kwa
utafiti.
Ernest Mangu ni
mkuu wa jeshi la Polisi nchini ambaye katika hotuba yake amesema nchi bado ipo
salama sana ukilinganisha na nchi jirani ambapo mkuu wa chuo cha taaluma ya
Polisi katika amesema waliohitimu ni askari 290 huku wanafunzi saba wakishindwa
kumaliza kutokana na sababu mbalimbali ikwemo utovu wa nidhamu.
Post a Comment