Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Gari alilotumia Nyerere kusaka Uhuru lakarabatiwa

Wananchi wakiliangalia gari lililotumiwa na Mwalimu Julius Nyerere katika harakati za kutafuta Uhuru wa Tanganyika likiwa katika Banda la Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kwenye maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa jana. Gari hilo limekarabatiwa na Chuo cha Veta Tawi la Moshi mwaka 2014. (Picha na Yusuf Badi).
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imekarabati gari alilokuwa akitumia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kutafuta uhuru kabla ya mwaka 1961.
Gari hilo aina ya Austin iliyotengenezwa mwaka 1947 hadi 1956 nchini Uingereza, lilikuwa la Aminadabu Solomon Nkya ambaye alimpa Nyerere kutembelea kudai uhuru.
Akizungumza katika viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya 39 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere maarufu kama Sabasaba, Mkufunzi wa Chuo cha VETA mkoani Kilimanjaro, Hurbert Makundi, alisema chuo hicho kimekarabati gari hilo kwa lengo la kumuenzi Nyerere aliyekifungua mwaka 1984.
Alisema wamelikarabati gari hilo lililokuwa limekufa kabisa na kutelekezwa katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka jana kazi iliyofanyika kwa miezi sita na kurudi katika hali ya kawaida na sasa linawaka.
Alisema baada ya maonesho wanatarajia kulikabidhi serikalini kupitia CCM Mkoa ili kulihifadhi kama kumbukumbu, huku wakitarajia kukarabati lingine ambalo nalo lipo mkoani humo.
Gari hilo limekuwa kivutio kwa watu wanaotembelea banda hilo na maonesho kwa ujumla kutokana na muundo wake wa kizamani, lakini sasa linaonekana kuwa jipya.
Baadhi ya wananchi waliotembelea maonesho hayo wameomba Serikali kulipeleka gari hilo katika Makumbusho ya Taifa kama yalivyowekwa mengine.
Mwananchi Gasper Mlay alisema gari hilo la kipekee ambalo huwezi kukutana nalo, kupelekwa makumbusho ya Taifa kutafanya vizazi vijavyo kupata mafunzo ya magari aliyotumia Mwalimu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top