Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe
(kushoto) akimkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CHADEMA, Waziri Mkuu
Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa mara baada ya
kujiunga na Chama hicho jioni hii kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Bahari
Beach, Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe
(kushoto) akimpongeza Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli,
Mh. Edward Lowassa mara baada ya kujiunga na Chama hicho jioni hii
kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Bahari Beach, Jijini Dar es Salaam.
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa na Mkewe
Mama Regina Lowassa wakionyesha kazi zao za CHADEMA mara baada ya
kujiunga rasmi jioni hii. CHANZO OTHMANI MICHUZI
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akiingia
kwenye ukumbi wa mikutano ndani ya hotel ya Bahari Beach jijini
Dar,kwenye mkutano wa Wanahabari jioni ya leo.
Mh.Lowassa akiingia kwenye Hoteli Bahari Beach kwa ajili ya kutangaza adhima yake ya kujiunga na UKAWA. Waziri
Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa ametangaza kujiunga rasmi na Umoja wa
Katiba (UKAWA) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) .
Mh.Lowassa
akiwa na viongozi wa UKAWA katika Hoteli ya Bahari Beach Hoteli jijini
Dar es Salaam jioni ya leo mara baada ya kutangaza rasmi azma yake ya
kujiunga na ukawa.
Mwenyekiti
wa Taifa wa Chadema,Freeman Mbowe akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu
Edward Lowassa katika Hoteli ya Bahari Beach Jijini Dar es Salaam jioni
hii alipokuwa akitangaza azma yake ya kujiunga na UKAWA kupitia chama
cha CHADEMA.
Mh.Waziri
Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa akiteta jambo na Mwenyekiti Taifa wa Chama
Cha Wananchi (CUF),Profesa Ibrahim Lipumba katika Hoteli ya Bahari
Beach jijini Dar es Salaam.
Post a Comment