Kwa
Nini UKAWA Wameamua LOWASSA Awe Mgombea wao wa Urais??.....
Tundu Lissu Amelijibu Swahi hili kwa Ufasaha Kabisa hapo chni:
Edward Lowassa anajiunga na CHADEMA na atakuwa mgombea urais wa CHADEMA na wa UKAWA. Lowassa is perhaps the most controversial and divisive political figure in the country right now.
Edward Lowassa anajiunga na CHADEMA na atakuwa mgombea urais wa CHADEMA na wa UKAWA. Lowassa is perhaps the most controversial and divisive political figure in the country right now.
Na
amekuwa hivyo kwa muda mrefu. Sisi CHADEMA tulimweka kwenye Orodha ya
Mafisadi kutokana na kuhusika kwake na Kashfa ya Richmond mwaka 2007.
Kwa
hiyo swali halali kabisa ambalo lazima tulijibu kwa ufasaha ni hili:
kwa nini tumekubali, sio tu kumpokea kama mwanachama, bali kumpa heshima
ya kuwa mgombea wetu wa urais.
Na
kwa nini washirika wetu wa UKAWA nao wamemkubali kuwa mgombea wao wa
urais??? Jibu ni kwamba tupo katika kipindi na mazingira ya kipekee ya
kisiasa katika nchi yetu. Kwa mara ya kwanza katika historia yetu kama
taifa, tunaona mfumo tawala ukipasuka vipande vipande.
Kwa
mara ya kwanza tunaona CCM ikipasuka katikati. Na mtu aliyeipasua CCM
na mfumo tawala ni Edward Lowassa. Sisi CHADEMA tumefanya kazi kubwa ya
kujenga chama tangu 2010.
Tuna
wagombea wengi na bora katika majimbo mengi ya uchaguzi na ngazi ya
madiwani kuliko ambavyo tumewahi kuwa nao kwa miaka yote ya nyuma. Hata
hivyo, ni ukweli pia kwamba kuna maeneo mengi ya nchi ambako tuko dhaifu
sana.
Kwa kuingia kwake CHADEMA na UKAWA, Lowassa anayaingiza maeneo hayo kwenye ulingo wa kisiasa and very much within our reach.
Na
Lowassa ataiporomosha CCM kwa sababu ana nguvu kubwa ndani ya chama
hicho kuliko mwanasiasa mwingine yeyote. Katika mazingira ya sasa ya
kipekee, tunahitaji kuamua nani ni adui mkubwa zaidi wa nchi yetu na
ustawi wake:Edward Lowassa mtuhumiwa wa ufisadi au CCM na mfumo tawala
ambao unajenga mazingira yanayostawisha na kulinda ufisadi.??
Sisi Chadema na UKAWA tumeamua kuwa adui yetu mkubwa wa sasa na siku zote ni CCM na mfumo tawala.
Sisi Chadema na UKAWA tumeamua kuwa adui yetu mkubwa wa sasa na siku zote ni CCM na mfumo tawala.
Tumemkaribisha
Edward Lowassa kwa sababu kuwepo kwake kutaharakisha kuiangamiza CCM na
mfumo tawala. Tunaomba wananchi mtuelewe na kutuunga mkono.
Post a Comment