Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Lowassa Asukiwa Zengwe Ili Jina Lake LIKATWE .... Wananchi wasubiri akatwe ili waikate CCM Octoba 25



Wakati joto la uchujaji wa majina ya wagombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) likizidi kuongezeka, taarifa zimezidi kuzagaa mitaani na kwenye mitandao ya kijamii kwamba, mikakati ya kumuondoa Edward Lowassa kwenye orodha ya watia nia nayo imezidi kupamba moto.
 
Ofisa mmoja wa CCM makao makuu mjini hapa, alisema kuwa wanachofanya wao kama watendaji ni kuandaa majina ya wagombea wote na fomu zao za udhamini na kisha kukabidhi kwa sekretarieti itakayopanga ajenda za vikao vya Kamati Kuu na baadaye Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya taifa.
 
Ofisa huyo alipoulizwa kama ana taarifa za kuwako kwa mizengwe dhidi ya Lowassa alisema kwa ujumla kwa sasa kuna maneno mengi sana yanazungumzwa juu ya mchakato wa uteuzi wa mgombea, ila akasisitiza kuwa la msingi ni kusubiri vikao vya maamuzi.
 
“Ndugu yangu ukiyatazama haya makundi (ya urais) ni vigumu kuamini kama wanatoka chama kimoja. Yaani kuna kukamiana kweli kweli…Kila mmoja anataka kumwangusha mwenzake ili yeye apite,” alisema na kuongeza kuwa:
 
“Hata kama kuna mizengwe, si unajua uchaguzi huu ni wa vyama vingi. CCM haishindani pekee yake, kwa hiyo mgombea anayekubalika ndiye anatakiwa.”
 
Hata hivyo, kwa muda sasa kumekuwa na mfululizo wa habari za kupikwa kwamba jina la Lowassa litaishia Kamati Kuu kwa madai kwamba kuna ushahidi wa matumizi ya fedha kwa timu yake, tuhuma ambazo binafsi (Lowassa) amezikanusha mara kadhaa.
 
Julai mosi mwaka huu siku anarejesha fomu za kuwania urais kupitia CCM alitoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa kuhusika kwake na rushwa ajitokeza na kusema alitoa lini, wapi na kwa nani.
 
Lowassa alisema amechoka kwa tuhuma za kipuuzi za kuhusishwa na rushwa na kusisitiza kuwa hakuna mwanachama yeyote miongoni mwa zaidi ya nane waliomdhamini aliyefanya hivyo kwa kishawishi cha fedha au fadhila yoyote.
 
Mgombea anayetajwa kutumiwa zaidi na kundi linalompinga Lowassa ni pamoja na Makongoro Nyerere, ambaye alifanya mkutano na waandishi wa habari hivi karibuni na kuporomosha kauli kali za ukakasi dhidi ya Lowassa.
 
Wakati mizengwe ikizidi kusukwa dhidi ya Lowassa, ripoti ya kura zote za maoni ambazo zimekuwa zikitolewa katika miezi ya hivi karibuni zimeonyesha kuwa Lowassa anaongoza kwa mbali kama chaguo la wananchi wengi kwenye nafasi hiyo.
 
Miongoni mwa tafiti hizo ni ule wa Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia (REDET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, uliofanywa mwezi uliopita na matokeo yake kutolewa mwishoni mwa wiki unaonyesha kuwa Lowassa ni changuo la kwanza la wengi kwa kujipatia asilimia 27.0 ndani ya chama hicho, huku Bernard Membe akishikilia nafasi ya pili kwa kupata asilimia 8.2.
 
Katika utafiti huo ambao REDET walisema kuwa unaweza kuchukuliwa kwa ujumla wake kama maoni ya Watanzania endapo masuala yaliyoulizwa uchaguzi ungefanyika katika kipindi cha utafiti, wahojiwa walikuwa 1,250 kutoka wilaya moja moja katika mikoa 25 ya Tanzania Bara.
 
Wakati mkakati wa mizengwe ukiendelea kupamba moto, wajumbe wa sekretarieti ya Kamati Kuu ya chama hicho wanaanza vikao mjini Dodoma leo kundaa pamoja na mambo mengine ajenda na taarifa kwenye vikao vya Kamati Kuu itakayokaa Alhamisi mjini hapa.
 
Kikao cha Kamati Kuu kinatarajiwa kuchuka majina ya watia nia 38 waliojitokeza kutafuta ridhaa ya chama hicho na kubakisha majina matano tu yatakayopelekwa NEC kwa kupigiwa kura.
 
NEC inayotarajiwa kukutana Ijumaa wiki hii, itatoa majina matatu kwenda Mkutano Mkuu unaotarajiwa kukutana Jumamosi kwa ajili ya kupata jina moja la mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top