WE acha
tu! Hii ni habari ya kushangaza sana ambayo ilinaswa na paparazi
juzikati ambapo mwanaume aliyefahamika kwa jina la Ally Mwamwanza ambaye
ni afisa katika kitengo cha ‘makontena’ bandarini Dar, kudaiwa kunaswa
na mke wa jirani yake, Gibson Mtinge aliyetajwa kwa jina moja la
Khadija.
Ally Mwamwanza akidhibitiwa baada ya fumanizi hilo.
Licha
ya wote wawili kuishi Mbezi ya Kimara, lakini kisanga hicho kilichojiri
mwishoni mwa wiki iliyopita saa 12 asubuhi kilichukua nafasi maeneo ya
Tegeta-Kibaoni jijini Dar es Salaam.
Ilikuwa
katika pilikapilika ya kusaka matukio ya usiku katika viwanja
mbalimbali vya Jiji la Dar. Wakati inapita nje ya nyumba hiyo, kelele za
‘hoya! Hoya’ ziliifanya kuzama
ndani ya mjengo huo wa maana na kukutana na kasheshe ya mwaka, wanaume
wawili wakitwangana.Mwanaume aliyejitaja kuwa ni mfanyabiashara wa
kusafirisafiri ambaye ndiye Gibson alidai amemfumania Ally akiwa na
mkewe kitandani kwenye chumba kimoja ndani ya nyumba hiyo.
“Huyu
jamaa nimemkuta na mke wangu. Huwezi kunifanyia hivi bwana Ally. Halafu
wewe ni jirani yangu kabisa,” alifunguka Gibson kwa sauti yenye kuweza
kufanya lolote kwa wakati huo kama si Mungu kumdhibiti shetani.
MTUHUMIWA ALITOKA KWAKE MUDA WA DAKU
Habari zaidi kutoka kwenye kinywa cha Gibson zilisema kuwa, Ally alikuwa akimtongoza mkewe kwa siku nyingi. Ikafika mahali, mke huyo akachoka na kumweleza mumewe ambapo waliweka mtego.
Habari zaidi kutoka kwenye kinywa cha Gibson zilisema kuwa, Ally alikuwa akimtongoza mkewe kwa siku nyingi. Ikafika mahali, mke huyo akachoka na kumweleza mumewe ambapo waliweka mtego.
Siku
hiyo, inadaiwa Ally alichati na mwanamke huyo akitaka waonane, mke
akamwambia hayupo Mbezi wanapoishi, amelala Tegeta kwenye nyumba ya dada
yake kwa vile dada huyo amekwenda Mbeya. Kwa hiyo kama anataka yeye
aende Tegeta.
Akiomba kuachiwa.
“Jamaa
katoka kwake Mbezi saa 10 alfajiri, muda ambao watu wanakula daku kwa
ajili ya mfungo. Alimuaga mkewe anakwenda kazini,” alisema Gibson huku
akivuja jasho maana Ally naye ni bonge.
Ina maana taarifa hizo, Gibson alipewa na mke wake ambaye alikuwa akichati na Ally!
Ina maana taarifa hizo, Gibson alipewa na mke wake ambaye alikuwa akichati na Ally!
MAJIRANI WAINGILIA KATI
Majirani wa eneo hilo, baada ya kusikia sekeseke walizama ndani na kufanya kazi ya ziada kuwatuliza na kumtaka Gibson amwache Ally avae nguo.
Majirani wa eneo hilo, baada ya kusikia sekeseke walizama ndani na kufanya kazi ya ziada kuwatuliza na kumtaka Gibson amwache Ally avae nguo.
MTUHUMIWA AJIPIGA FAINI
Baada ya vuta nikuvute iliyochukua muda wa saa 3, Ally alikiri kutenda kosa hilo na hivyo kuamua kujipiga faini mwenyewe kwa kusema atampa jamaa huyo mwenye mke kiasi cha shilingi milioni 30 kama fidia ya ugoni.
Ally akiyaweka maelezo yake hayo kwenye karatasi na kuanguka ‘signecha’ huku akitazamwa na mashahidi wawili ambao nao walimwaga wino.
Baada ya vuta nikuvute iliyochukua muda wa saa 3, Ally alikiri kutenda kosa hilo na hivyo kuamua kujipiga faini mwenyewe kwa kusema atampa jamaa huyo mwenye mke kiasi cha shilingi milioni 30 kama fidia ya ugoni.
Ally akiyaweka maelezo yake hayo kwenye karatasi na kuanguka ‘signecha’ huku akitazamwa na mashahidi wawili ambao nao walimwaga wino.
Post a Comment