Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TID: Ni Kweli Navuta Bangi


Kwa mara ya kwanza, ‘mnyama’ katika anga la muziki wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘Top In Dar’ (TID) amekiri kutumia mihadarati aina ya bangi huku akijiapiza kuwa hajawahi kutumia madawa mengine ya kulevya ‘unga’ ikiwemo cocaine kama ambavyo amekuwa akinyoshewa vidole na baadhi ya watu.

Akizungumza na Gazeti  la  Ijumaa katika mahojiano maalum wikiendi iliyopita, TID ambaye ni mmiliki wa Top Band alifunguka kuwa miongoni mwa mambo yanayomkosesha raha na amani ya moyo, ni pamoja na kuhukumiwa kujihusisha na matumizi ya unga na wengine kwenda mbele kwa kusema hata kushuka kwake kisanii kumechangiwa na ishu hiyo.

Staa huyo wa Ngoma ya Kiuno alisema kuwa, wakati mwingine watu wanamsakama hadi mama yake mzazi wakimtaka amkanye mwanaye kujiepusha na maisha ya ‘kubwia unga’ jambo ambalo linampa wakati mgumu na kujiona kuonewa katika jamii.

Kuhusu kushuka kimuziki, TID alisema miongoni mwa sababu zilizosababisha kuporomoka katika anga la muziki ni kile alichokiita ‘hujuma’ kutoka kwa baadhi ya wadau wakubwa wa muziki (majina yapo), kwa kushindwa kumpa fursa za kimuziki zikiwemo promosheni na mialiko ya shoo kwa kuwa wana vinyongo na fitina dhidi yake.

“Kaka, naonewa kabisa nikihusishwa natumia madawa ya kulevya, wanamsumbua mama eti akae na mimi anionye.

“Jamani situmii madawa ya kulevya kama cocaine, ila kwa upande wa bangi ni sawa nakubali kuwa navuta.

“Lakini pia, kuvuta kwangu bangi siyo sababu ya mimi kushuka kisanii, zipo sababu zingine kabisa kama kuhujumiwa na wadau wakubwa wa soko la muziki kutokana na mabifu yanayotokana na sababu binafsi.

“Hivi kweli mtu anayetumia madawa ya kulevya kama cocaine, anaweza kumudu maisha kama kununua nyumba? Kununua magari? Hata kuendelea kuimba kweli? Siyo sawa jamani,” alisema TID.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top