Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Urais 2015: UKAWA Waahidi Neema Kwa Wachimbaji



SERIKALI itakayoundwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) imeahidi kuwapa kipaumbele wachimbaji wadogowadogo ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo katika shughuli za uchimbaji wa madini huku ikihakikisha kuwa kampuni kubwa za uwekezaji zikilipa kodi stahiki ya Serikali.
 
Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahimu Lipumba, alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Kahama katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja CDT mjini hapa.
 
Lipumba alisema kuwa kwa sasa Serikali imekuwa haiwajali wachimbaji wadogowadogo wa madini hususani wa madini ya dhahabu ambapo wamekuwa wakigundua maeneo yenye madini kisha baadaye huondolewa na Serikali kwa kile kinachodaiwa kuwa hawana leseni za kumiliki maeneo hayo.
 
Alisema kuwa wachimbaji hao wamekuwa waathirika kila wanapoibua maeneo ya mgodi kwani hutolewa badala ya Serikali kuwajengea uwezo wa uchimbaji pamoja na kuwaongezea mitaji hali ambayo ingesaidia kupunguza kukosekana kwa ajira tatizo ambalo ni kubwa kwa vijana nchini.
 
Aidha Lipumba aliitaka Serikali kutokuwakumbatia wawekezaji wakubwa hasa wa madini na kuwasahau wale wadogo ambao ndio chanzo cha kupatikana kwa maeneo ya uchimbaji na kuwa chanzo cha kukua kwa miji midogo katika maeneo ya uchimbaji wa madini.
 
Pamoja na mambo mengine Lipumba alisisitiza kwa Serikali kuwatafutia wakulima wa zao la tumbaku na pamba masoko ya uhakika yatakayoleta tija kwa wakulima na kuondokana na malalamiko yaliyopo kwa wakulima wa mazao hayo kwa sasa katika Kanda ya Ziwa.
 
Pia Lipumba alisema Ukawa itakapoingia madarakani haitatoa nafasi kwa kampuni kubwa kusamehewa kodi kwani kwa kufanya hivyo kunarudisha nyuma maendeleo ya taifa na kukosekana pato ambalo linaweza kuwasaidia wajasiriamali wadogo ambao hawana kipato kwa sasa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top