Msanii wa muziki wa Bongo Flava Sunday ‘Linex’ Mjeda, ameamua kuelezea mkasa uliomkuta baada ya ‘kuikwangua’ gari ya mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda wiki tatu zilizopita.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook,Linex ameelezea Ikhsani aliyofanyiwa na Makonda licha ya kumfanyia makosa.
Usome ujumbe wake hapo chini then tuachie maoni yako.
“Katika
mizunguko ya hapa na pale Kama week mbili tatu zilizo pita majira ya
saa 9:00 usiku kwa bahati mbaya nilipiga pasi gari la mtu nikashuka kwa
lengo LA kufanya makubaliano nae mala nikashangaa ameshuka mh
@paulmakonda kwa kua sijawahi kukaa nae kokote wala kufahamiana nae
nikajua Leo yamenifika lakini cha kushangaza aliposhuka
Aliangalia
wapi pamekwaruzika then akaniambia ni bahati mbaya wakati mi nilijua
atatumia nguvu au nafasi aliyo nayo serikalini kweli usiamini
unachosikia au kuona hata chumvi saa nyingine hua Ina fanana na sukari
#TheVOA” ameandika Linex.
Post a Comment