Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Maelezo ya Mtatiro kuhusu kesi ya kupinga ushindi wa CCM Segerea



Napenda kutoa taarifa hii rasmi na ya awali kwa wananchi wa Segerea na watanzania wote ambao walipigana kufa na kupona ili kuhakikisha UKAWA tunashinda madiwani, mbunge na kuongoza kura za Rais hapa jimboni. Kwa bahati mbaya tulifanikiwa kushinda madiwani wote, kuongoza kura za Rais lakini tukashindwa kwenye Ubunge.
 
Baada ya jimbo letu kwenda CCM nilishauriwa nisisaini kukubali matokeo na nikatekeleza ushauri huo, lengo lilikuwa ni kuwapa muda wanasheria wetu na mawakili waweze kushauri ikiwa kuna kesi ya kufungua kupinga ushindi wa CCM.
 
Baada ya mashauriano ya wiki kadhaa yaliyohusisha mawakili na wataalam wa sheria wa ngazi mbalimbali, tumejiridhisha na kushauriwa kwamba hatutakuwa na kesi ya kufungua, na kwamba tukiifungua kwa kulazimisha au "kwa kusukumwa na upepo wa wananchi" tutashindwa mahakamani mapema.
 
Wanasiasa wengi hukimbilia mahakamani wanaposhindwa uchaguzi si kwa sababu wana kesi zenye ushahidi wenye mashiko, bali huogopa maneno na tuhuma wanazoweza kupewa kuwa "wamenunuliwa na wagombea wa CCM", mimi kwa bahati nzuri sijakumbwa na upepo huo na natambua wananchi wa Segerea wananiamini kiasi cha kutosha.
 
Baada ya wiki moja kutoka sasa, ntatoa taarifa rasmi na ya kina juu ya hoja na sababu zilizopelekea wanasheria na mawakili wetu washauri tusihangaike kufungua kesi na kupoteza muda wa matumaini ya wananchi.
 
Mtatiro Julius,
Segerea.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top