Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MKEMIA MKUU WA SERIKALI AANDAA WARSHA


Beatrice Lyimo,Dar es Salaam.

Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeandaa warsha ya mafunzo juu ya kujiandaa kukabiliana na dharura ya kemikali hatari na zenye madhara kwa afya na mazingira kwenye maeneo ya bandari.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mkemia mkuu wa serikali Prof. Samweli Manyele amasema kuwa lengo la warsha ya mafunzo hayo ni kuwasilisha na kusambaza matokeo ya utafiti kwa kuhamasisha matumisi salama ya kemikali katika ukanda wa afrika.

“kufundisha nchi za ukanda wa Afrika Mashariki juu ya namna ya kushughulika na kusimamia kemikali hatari na zenye madhara, namna ya kujiandaa na kukabiliana na matukio ya kemikali pamoja na kubadilisha uzoefu wa ushughulikiaji salama wa kemikali hizo kati ya nchi na nchi” aliongeza Prof Manyele.

Pia kujadili mahitaji ya nchi na kikanda pamoja na kutambua hatua za kuelekea njia bora Zaidi ya kujianda na kukabiliana na matukio ya kemikali katika maeneo ya bandari na njia za usafirishaji ni moja ya lengo ya warsha hiyo.

“Ni matumaini yangu warsha ya mafunzo hayo yatakuwa muhimu katika kuongeza uelewa wa washiriki na kujenga uwezo wao wa kushughulikia mizigo ya kemikali hatari kwa usalama na hivyo kulinda afya, mazingira na mali dhidi ya madhara ya kemikali hizo” alifafanua Prof. Manyele.

Warsha hiyo itafanyika kwa muda siku mbili kuanzia tarehe 26 hadi 27 Noverma, 2015 kwenye ukumbi wa Protea Courtyard Hotel iliyopo jijini dar es salaam na kuhusisha nchi mbalimbali.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top