Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TID AANIKA MAHUSIANO YAKE NA WEMA SEPETU


Msanii mkongwe wa muziki, TID amesema kipindi cha nyuma alikuwa anatoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu lakini baadae alitemwa hali ambayo ilimuumiza sana.

Akizungumza katika kipindi cha Clouds TV Ijumaa hii, TID amesema hali hiyo ilimfanya atoke na wasichana wengi.

“Nilikuwa ‘namdate’ Wema Sepetu akaniambia sikutaaki, tangu kipindi hicho nimekuwa na wasichana wengi. Ikitokea Wema anataka kurudi hakuna nafasi, I’m occupied,” alisema TID.

TID amesema katika kipindi hicho aliumizwa sana na jinsi magazeti yalivyokuwa yanamuandika vibaya.

“Wakati huo mitandao ya kijamii haikuwepo lakini wamagazeti walizichukua picha na kufanya yao, it was bad. Mimi nikasema sawa lakini niliumia sana,” alisema TID.

Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Confidence’ aliyomshirikisha Joh Makini pamoja na Dully Sykes.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top