Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BOMOA BOMOA YAENDELEA KWA KASI

Wakazi waliojenga eneo la Iloganzila Jimbo la Kibamba Dar es salaam leo wamebomolewa nyumba zao ambazo ni zaidi ya nyumba 400, zoezi hilo limekuja baada ya amri iliyotolewa na Mahakama Kuu juzi.

Taarifa zinasema eneo hilo lenye ukubwa wa heka 33, mali ya Henry Kashangaki lilikuwa na mgogoro tangu 1997 baada ya kundi la watu 11 kuvamia na kuanza kujenga nyumba na kuwauzia wananchi wengine.

Baada ya eneo hilo kuvamiwa mmiliki wake aliamua kwenda mahakamani na kuwashtaki Shaha Matibwa na wenzake kumi, kesi hiyo iliendeshwa kwa muda wa miaka mitano na mwaka 2010 hukumu ilitolewa na Kashangaki na Matibwa walionekana wana haki ya kumiliki hivyo walitakiwa kugawana.

Hata hivyo, Kashangaki hakuridhika na hukumu hiyo na kukata rufaa na kwenda Mahakama Kuu, January 2016 kesi hiyo ilitolewa hukumu na Kashangaki alishinda, hivyo juzi Mahakama hiyo ilitoa amri nyumba zivunjwe ili kumpisha mwenye eneo lake.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top