Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MBOWE NA VIONGOZI WENGINEO WA KITAIFA WA CHADEMA WAZUIWA KUINGIA OFISINI

Viongozi na makada wa Chadema waliokuwa wakisafiri kutoka Kahama kuelekea jijini Mwanza jana wamejikuta wakishindwa kuingia kwenye ofisi za chama hicho mjini Shinyanga kutia saini kitabu cha wageni baada ya Jeshi la Polisi kuzuia shughuli yoyote ya chama hicho mjini humo.

Waliokumbwa na adha hiyo ni pamoja na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk Vicent Mashinji na wabunge Godbless Lema, Ester Bulaya, John Heche, Halima Mdee na viongozi kadhaa wa kitaifa wa Chadema.

Magari manne ya polisi yaliyosheheni askari waliobeba silaha na mabomu ya kutoa machozi yaliupokea msafara wa Chadema uliokuwa ukielekea Mwanza, mara tu ulipoingia mjini Shinyanga na kuusindikiza hadi nje ya mji kuhakikisha hausimami ndani ya mji huo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top