Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MUGABE ANA VINA SABA VYA KUISHI MILELE

 Rais wa Zimbabwe, Komrade Robert Mugabe

WANASAYANSI maarufu kutoka Taasisi moja kubwa ya Sayansi nchini Uingereza wametoa ripoti ya utafiti walioufanya ikithibitisha kwamba, Rais wa Zimbabwe, Komrade Robert Mugabe amegundulika kuwa na vinasaba (genes) ambavyo vitamfanya aishi milele (asife).

Robert Mugabemiaka ya 1980.

Utafiti huo wa siri unaongozwa na Daktari Irvin Koch umegharimu mabilioni ya fedha na kugundua pia kwamba Bob Robert mwenye miaka 92 sasa haweki dawa kichwani (SUPER BLACK) wala hajawahi kukata nywele zake licha ya kutojihangaisha na kula vyakula vya mimea (veggies) ama kwenda gym kufanya mazoezi.

Katika tafiti hiyo, Wanasayansi hao walichukua sampuli mbalimbali kutoka kwa Bob ikiwemo damu yake, nguo zake, miswaki aliyokuwa akitumia, na hata chanuo kwa miongo kadhaa na kugundua kuwa hakuna hata chembe ya umauti kwa Mugabe.
Baadhi ya watu wameanza kuamini kuamini tafiti hizo baada ya kugundua kutoka kwenye picha za Mugabe akiendelea kupeta katika muonekano huohuo huku akiwa mwenye siha ya haja kwa miaka mingi sasa.

Mpinzani wake mkuu kwenye siasa za Zimbabwe ambaye ni Kongozi wa Chama cha MDC, Morgan Tsvangirai (ama kwa kuguswa kwamba ausahau uraisi) amejibu kwa kejeli kwamba ‘Mugabe ni makusanyo ya nyama na mifupa kama hayawani wengine wote’ na kwamba kila nafsi itaonja mauti (Kulu ‘nafsi dhaaikatul ‘maut).
Inasemekana kwamba utafiti huo unaendelea mpaka mwaka 2018 ndipo utakamilika.
Source: Newssa/Mzansi Satire
Zimbabwe News Day===http://bit.ly/1rlaUBX
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top