Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

AJALI MBAYA YAUA NA KUJERUHI WATU MKOANI LINDI

Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine amejeruhiwa vibaya katika ajali ya gari iliyotokea wilayani Kilwa mkoani Lindi baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso.

Taarifa ya jeshi la polisi mkoani Lindi imeeleza kuwa ajali hiyo ilitokea katika eneo la Kisangi katika kijiji cha Mkwanyule kwenye barabara ya Kilwa Lindi ambapo gari yenye nambari za usajili T 556 Suzuki Carry iliyokuwa ikiendeshwa na dereva Hijra Said Abdurahman ambae alifariki hapohapo baada ya gari yake kugongana uso kwa uso na gari nyingine Toyota Corolla yenye nambari za usajili T 840 Bug iliyokuwa inaendeshwa na Ahmad Mohamed Mfaume ambae amejeruhiwa katika paji lake la uso.

Mkuu wa wilaya ya Kilwa Christopher Ngubiagai amezungumzia kuhusu ajali hiyo na akatoa wito kwa madreva kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kukomesha matukio ya ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara na kusababisha vifo vya raia na uptevu wa mali.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top