Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HALMASHAURI KUU YA CCM YAKETI KUPENDEKEZS JINA LA DK. MAGUFULI KUWA MWENYEKITI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimuongoza Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kuingia ukumbini, kwa ajili ya kuendesha kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) leo katika ukumbi wa Sekretarieti uliopo katika Jengola White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, leo. Wanaofuata ni Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa , Rais Dk. John Magufuli na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa ,Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein. Kikao hicho kilikuwa na ajenda moja, ya kupokea jina la Rais Dk. Magufuli ili kuliafiki au kulikataa kuwa Mwenyekiti wa CCM wa awamu ya tano kufuatia Mwenyekiti wa sasa atakapostaafu na kumwachia kijiti cha uongozi huo wa Chama katika mkutano mkuu maalum wa CCM utakaofanyika kesho katika Ukumbi wa Dodoma Convetion.
 Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan (kuashoto) akiingia ukumbini kushiriki katika kikao hicho
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete akiongoza shamra shamra baada ya yeye na viongozi wenzake kuwasili ukumbini kwa ajili ya kikao hicho
 Wajume wakiwa wamesimama kumlaki Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete baada yeye na viongozi wenzake kuwasili ukumbini kwa ajili ya kikao hicho cha NEC
Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na viongozi wenzake wakiwa tayari meza kuu kuendesha kikao hicho. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM, mtarajiwa Rais Dk John Magufuli, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein na kulia niMakamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
 
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, kilichofanyika leo. Kulis ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Mweyekiti wa CCM mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein wakati wa kikao hicho cha NEC kilichofanyika leo.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein akijadili jambo na Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa, Rais Dk. John Magufuli wakati wa kikao hicho cha NEC kilichofanyika leo.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhwavi akitoa taarifa ya maandalizi ya mkutano mkuu maalum wa CCM utakaofanyika kesho, Julai 23, 2016, wakati wa kikao hicho cha NEC. 
 Wajumbe wa NEC na Wajume waalikwa wa NEC, wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kulia ni Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Raijab Luhwavi, Katibu wa NEC Oganaizesheni Mohammed Seif Khatib na Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakia Hamdan Meghji
 Katibu wa NEC Itikasi na Uenezi na Msemaji Mkuu wa CCM, Christopher Ole Sendeka wakijadiliana jambo wakati wa kikao hicho cha NEC
  Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana wakati wakijadili jambo wakati wa kikao hicho cha NEC kilichofayika leo
 Kiti alichokuwa amekalia Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli (kushoto), kikiwa wazi baada ya Dk. Magufuli kutoka ukumbi kutoa nafasi ya jina lake kutajwa na Mwenyekiti wa CCM Dk Jakaya Kikwete (wapili kushoto), kwa wajumbe wa NEC leo, Kama lilivyopendekezwa na Kikao Cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika jana kwa kumpendekeza Dk. Magufuli kuwa Mweneyekiti wa CCM wa awamu ya tano. Kulia ni Makamu Kwenyekiti wa CCM Bara na Katibu Mkuu wa CCM Abduulrahman Kinana
 Wajumbe wa NEC wakiwa wamenyoosha mikono kushirikia kulipitisha jina la Rais Dk. Magufuli kuwa Mwenyekiti wa CCM, kufuatia kulipitisha, jina hilo kesho litapelekwa kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa CCM ili kupigiwa kura ya ndiyo au hapana.
 Wajumbe wa NEC wakiwa wamenyoosha mikono kushirikia kulipitisha jina la Rais Dk. Magufuli kuwa Mwenyekiti wa CCM, kufuatia kulipitisha, jina hilo kesho litapelekwa kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa CCM ili kupigiwa kura ya ndiyo au hapana.
 Viongozi wa Meza Kuu wakiwa wamesimama kuwaunga mkono wajumbe waliosimama na kuamsha shamrashamra baada ya jina la Rais Dk John Magufuli kupitishwa na wajumbe katika kikao hicho cha NEC
 Wajumbe wakiwa wamesimama kwa shamrashamra hizo
 Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli akitoa neno la shukurani baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe wa NEC wakati wa kikao hicho cha NEC
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete akimpongeza, Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli baada ya maelezo yake mazuri wakati akitoa neno la shukurani baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe wa NEC
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein,akimpongeza, Mwenyekiti wa CCM mtarajiwa Rais Dk. John Magufuli baada ya maelezo yake mazuri wakati akitoa neno la shukurani baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe wa NEC 
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akionyesha katarasi itakayotumiwa na wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM kupiga kura 
 Juma Borafya kutoka Zanzibar akisimama baada ya kuteuliwa kukubali au kukataa jina la Dk. Magufuli litakapowasilishwa kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa CCM
 Mjumbe wa NEC, Waziri Kiongozi Mstaafu, Shamsi Vuai Nahodha akitoa neno la shukrani mwishoni mwa kikao hicho.
 Makatibu wa NEC wakiwa kazini kuhakikisha kila jambo la muhimu  la kwenye kikao hicho linanukuliwa vema.
 Wajumbe wakiwa amejaa ukumbini
 Mweneyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete akimpongeza Nahodha kwa neno lake la shukurani
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akionyesha furaha yake kabla ya kufunga kikao hicho baada ya ajenda kumalizika hatua kwa hatua.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akikifunga kikao hicho cha NEC ambacho ni cha mwisho kwake kama Mwenyekiti, PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO, KWA PICHA NYINGINE KEM-KEM ZA KIKAO HICHO >>GONGA HAPA
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top