Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS MAGUFULI AMPA ULAJI MREMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyopewa amefanya uteuzi wa viongozi na watendaji wa taasisi mbalimbali za Serikali, na pia amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;
  1. Augustino Lyatonga Mrema.
  • Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole kwa kipindi cha miaka mitatu, kuanzia leo tarehe 16 Julai, 2016.
  • Augustino Lyatonga Mrema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Mhe. Eusebia Nicholaus Munuo ambaye muda wake umemalizika.
  1. William R. Mahalu
  • Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.
  1. Mohamed Janabi
  • Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
  1. Angelo Mtitu Mapunda
  • Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
  1. Sengiro Mulebya
  • Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
  1. Oliva Joseph Mhaiki
  • Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
  1. Winifrida Gaspar Rutaindurwa
  • Ameteuliwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.
  1. Charles Rukiko Majinge
  • Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.
  1. Julius David Mwaiselage
  • Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

Kupandishwa Vyeo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa 25 wa Jeshi la Polisi kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) na kuwa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP).

Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;

  1. Essaka Ndege Mugasa
  2. Adamson Afwilile Mponi
  3. Charles Ndalahwa Julius Kenyela
  4. Richard Malika Revocatus
  5. Geofrey Yesaya Kamwela
  6. Lucas John Mkondya
  7. John Mondoka Gudaba
  8. Matanga Renatus Mbushi
  9. Frasser Rweyemamu Kashai
  10. Ferdinand Elias Mtui
  11. Germanus Yotham Muhume
  12. Fulgence Clemence Ngonyani
  13. Modestus Gasper Lyimo
  14. Mboje John Shadrack Kanga
  15. Gabriel G.A. Njau
  16. Ahmed Zahor Msangi
  17. Anthony Jonas Rutashubulugukwa
  18. Dhahir Athuman Kidavashari
  19. Ndalo Nicholus Shihango
  20. Shaaban Mrai Hiki
  21. Simon Thomas Chillery
  22. Leonard Lwabuzara Paul
  23. Ahmada Abdalla Khamis
  24. Aziz Juma Mohamed
  25. Juma Yussuf Ally

Aidha, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi wengine 34 kutoka cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP).

Waliopandishwa vyeo hivyo ni kama ifuatavyo;

  1. Fortunatus Media Musilimu
  2. Goyayi Mabula Goyayi
  3. Gabriel Joseph Mukungu
  4. Ally Omary Ally
  5. Edward Selestine Bukombe
  6. Sifael Anase Mkonyi
  7. Naftari J. Mantamba
  8. Onesmo Manase Lyanga
  9. Paul Tresphory Kasabago
  10. Dadid Mshahara Hiza
  11. Robert Mayala
  12. Lazaro Benedict Mambosasa
  13. Camilius M. Wambura
  14. Mihayo Kagoro Msikhela
  15. Ramadhani Athumani Mungi
  16. Henry Mwaibambe Sikoki
  17. Renata Michael Mzinga
  18. Suzan Salome Kaganda
  19. Neema M. Mwanga
  20. Mponjoli Lotson
  21. Benedict Michael Wakulyamba
  22. Wilbroad William Mtafungwa
  23. Gemini Sebastian Mushi
  24. Peter Charles Kakamba
  25. Ramadhan Ng’anzi Hassan
  26. Christopher Cyprian Fuime
  27. Charles Philip Ulaya
  28. Gilles Bilabaye Muroto
  29. Mwamini Marco Lwantale
  30. Allute Yusufu Makita
  31. Kheriyangu Mgeni Khamis
  32. Nassor Ali Mohammed
  33. Salehe Mohamed Salehe
  34. Mohamed Sheikhan Mohamed
Maafisa hawa wa Jeshi la Polisi Tanzania wamepandishwa vyeo kuanzia tarehe 15 Julai, 2016.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
16 Julai, 2016
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top