Ouma amekuwa akiishi na mmoja wa wasichana hao kuanzia mwaka wa 2008 kufuatia kifo cha mamake.
Mfanyabiashara mashuhuri kutoka katika kaunti ya Busia anasemekana kuwanajisi na kuwapachika mimba wasichana 9 wenye umri mdogo.
Joseph Ouma ambaye pia anasemekana kuwa na virusi vya ugonjwa wa ukimwi, alikiri kutekeleza kitendo hicho cha unyama akisema kuwa alifanya hivyo ‘ili kutibu hali yake ya HIV.’
Wasichana hao aliowanajisi na kuwapachika mimba ni wa darasa la tano, sita, na la saba kutoka shule ya msingi ya Morukeyan na ni wa kati ya umri wa miaka 10 na 17 .
Kulingania na habari za The star, Ouma amekuwa akiishi na mmoja wa wasichana hao kuanzia mwaka wa 2008 kufuatia kifo cha mamake.
Ouma sasa anasemekana kuwaambukiza wasichana hao wote virusi vya Ukimwi.
Aidha, imesemekana kuwa Ouma amekuwa akipeana hongo kwa wanakijiji ili kukwepa kuripotiwa kwa maafisa wa polisi.
Post a Comment