Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mwigulu awapasha UKAWA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amesema Jeshi la Polisi nchini linafanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu na linapomkamata mtu halimuulizi itikadi ya chama chake.
 
Waziri Mwigulu ameyasema hayo leo bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) kutoka Mwanza Susan Masele aliyetaka kupata kauli ya serikali juu ya askari polisi ambao wanawabambikizia kesi wafuasi wa UKAWA kwa kuwapa kesi za uchochezi.

“Jeshi la polisi linapowakamata watu, haliwaulizi itikadi zao, na linapowafikisha mahakamani haliwaulizi kadi za vyama vyao bali huangalia kosa ambalo limefanyika” Amesema Waziri Mwigulu.

Aidha waziri amesema kuwa wananchi wanaweza kupeleka malalamiko yao kuhusu Jeshi la Polisi katika vyombo vinavyoshughulikia sheria au katika makao makuu ya jeshi kwa kuwa kuna kitengo kinachoshuhulikia malalamiko ya wananchi.

Sambamba na hayo Waziri Mwigulu ameweka bayana kwamba askari ambao hukutwa na mashtaka ya kuwabambikizia wananchi kesi au mambo mengine na yakibainika kuwa ni ya kweli huadhibiwa na kulingana na sheria.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top