Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YATOA KAULI BUNGENI KUHUSU TETEMEKO LA ARDHI KAGERA



#Serikali yatoa msaada kwa waathirika kwa kuwapatia makazi ya muda baadhi ya wananchi ambao nyumba zao zimeathirika kwa majirani.

#Serikali imeelekeza wanajiolojia kutoa maelekezo ya kisayansi ili kuwatoa hofu wananchi kuhusu hali hiyo.

# Serikali imeongeza nguvu ya madaktari bingwa 15 toka mkoani Mwanza ili waweze kutoa huduma haraka kwa waathirika.

#Serikali imewahamasisha pia wananchi waweze kusaidiana pale inapowezekana.

#Serikali imewaagiza Wakurugenzi Manispaa ya Bukoba na Halmashauri ya Bukoba kufunga kwa mudw Shule za Ihundo Sekondari na Nyakato Sekondari kwa kuwa zina hali mbaya.

#Serikali inaendelea kuhakikisha hatua za dharura zinachukuliwa kwa kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha kuwa hatua za muda mfupi na muda mrefu zinatambuliwa na kutekelezwa ili kuwasaidia wahanga.

# Serikali inaendelea kufanya tathimini ya athari zilizosababishwa na tetemeko la ardhi.

# Serikali inaomba wadau wote wa Ndani na Nje wanaotaka kuchangia wawasiliane na *Ofisi ya Waziri Mkuu na Kamati ya Maafa ya Mkoa tu*.

#Serikali inatoa onyo kwa yeyote mwenye kutumia maafa haya kama sehemu ya kujinufaisha.

#Serikali imewataka wananchi kuwa wavulimivu na kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutatua tatizo ambalo limeipata nchi ili wananchi waendelee kupata huduma kulingana na athari za tetemeko.

#Waheshimiwa wabunge wameunga mkono juhudi hizo za Serikali na wameridhia kwa kauli moja kukatwa posho yao ya siku moja ili kuchangia maafa hayo.

*Imetolewa na Idara ya Habari-MAELEZO*
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top