Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Watu 66 wakamatwa kwa kukutwa na dawa za kulevya

Na John Nditi, Morogoro

JESHI la Polisi mkoani Morogoro limewatia mbaroni watu  66 kwa tuhuma za  makosa ya kupatikiana na dawa za kulevya aina za heroine, mirungi na bangi viroba 39.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakati  wa operesheni maalumu dhidi ya mapambano ya dawa za kulevya iliyofanyika kuanzia Februari 19, mwaka huu kutoka wilaya za mkoa wa  Morogoro.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, alisema  hayo Feb 20, mwaka huu ofisini mwake wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya  operesheni inayoendelea kufanyika kuhusu  mapambano dhidi ya dawa za kulevya  kwenye  wilaya  za mkoa huo.

Matei alisema , watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa na   watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili .
 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, akionesha kifurushi kilichohifadhi dawa za kulevya aina ya heroine iliyokamatwa  wakati wa oparesheni ya mapambano  dhidi ya  dawa za kulevya iliyofanyika  kuanzia Februari 18, mwaka huu  sambamba na ukamataji wa viroba 39  vya bangi pamoja  na mirungi  kama alivyokuwa akiwaonesha waandishi wa habari Februari  20, mwaka huu  kwenye  uwanja wa Jengo la Polisi la mkoa huo.
 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, akionesha kifurushi kilichohifadhi dawa za kulevya aina ya heroine iliyokamatwa  wakati wa oparesheni ya mapambano  dhidi ya  dawa za kulevya iliyofanyika  kuanzia Februari 18, mwaka huu  sambamba na ukamataji wa viroba 39  vya bangi pamoja  na mirungi  kama alivyokuwa akiwaonesha waandishi wa habari Februari  20, mwaka huu  kwenye  uwanja wa Jengo la Polisi la mkoa huo.
 Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, akitoa taarifa ya operesheni ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa waandishi wa habari , Februari 20, mwaka  huu ofisini kwake .
 Gari aina ya Totota Noah yenye namba za usajili T. 799 BUG ikiwa imeshikiliwa na Polisi baada ya kukmatwa ikisafirish  bangi  viroba 21 kutoka katika kijiji cha Lubungo, Kata na Tarafa ya Mikese, wilaya ya Morogoro kwenda Jijini Dar es Salaam.( Picha na John Nditi). 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top