Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Halmashauri ya Igonga yawakakali Kooni watumishi kuhusu Uchunguzi wa CAG


HALMASHAURI ya wilaya ya Igunga,Mkoani Tabora imesema haitasita kuwachukulia hatua za kisheria watumishi wote watakaokwamisha upatikanaji wa majibu ya hoja za ukaguzi kwa muda waliokubaliana na hivyo kusababisha Halmashauri hiyo kupata hati ya mashaka au hati chafu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Igunga,Mkoani Tabora,Peter Onesmo alitoa tahadhari hiyo kwenye mkutano maalumu wa baraza la madiwani wa Halmashauri kupitia hoja za ukaguzi wa CAG kwa mwaka 2015/2016 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri uliopo mjini Igunga.

“Na kama taarifa hiyo itakuja kwamba hatua hazijachukuliwa hatutasita kuwachukulia hatua wale ambao wametusababisha tuvuke ile tarehe tuliyoweka utekelezaji hatujauweka,kwa hiyo kama mtu atakuwa anajitakia hayo basi afike tu huko apime”alisisitiza Mwenyekiti huyo.

Aidha Mwenyekiti huyo hata hivyo alifafanua kuwa maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa huo kwamba watumishi wote wale watakaosababisha Halmashauri kuingia katika mahali kusikostahili,ni lazima watachukuliwa hatua za kisheria.

Akifungua mkutano huo maalumu,Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Agrey Mwanry alisisitiza kwamba watu pekee wenye mamlaka na madaraka ya kufanya maamuzi katika Halmashauri ya wilaya ya Igunga ni watu wanaoitwa Baraza la madiwani kutokana na wao kuwa ndiyo wawakilishi wa wananchi.

“Kwa nini leo kuna districk Commisioner na Region Commishiner hapa,Regional Comisioner na district Comisioner wanakuja hapa kama wawakilishi wa Rais kwa maneno mengine ni wawakilishi wa serikali,kwa nini kwa sababu Halmashauri ya wilaya ya Igunga inapokea ruzuku ya serikali”alifafanua Mwananry.

Hata hivyo Mkaguzi wa nje,Mohamed Msangi aliweka bayana kwamba bado utekelezaji wa maoni ya CAG siyo wa kuridhisha kwani kati ya hoja 120 zilizotolewa kwa hesabu za mwaka 2015/2016 zikijumulisha na hoja za miaka ya nyuma,ni hoja 72 tu zilizopatiwa majinu ya kuridhisha na kufungwa na hivyo hoja 48 sawa na asilimia 40 zimeendelea kusalia.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top