Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Sumaye 'aivaa' tena Serikali

Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani na Mjumbe wa Halmashauri  Kuu Chadema, Frederick Sumaye amesema kuwa licha ya kukatazwa wasizungumze masuala ya kisiasa, lakini hawatanyamaza.

Akizungumza na vyombo vya habari leo, Sumaye amesema kuwa wataendelea kufanya kazi kwa niaba ya wananchi ambao wana imani nao.

Amesema nchi  kwa sasa inakazana kujenga mfumo wa demokrasia kandamizi ambayo kwa kiasi kikubwa inarudisha nyuma maendeleo.

"Viongozi wa upinzani wamekuwa wakikamatwa, wanawekwa rumande, wanatishwa lengo ni kudhoofisha upinzani," amesema Sumaye.

Amesema licha ya juhudi hizo za kuwarubuni baadhi ya viongozi wakiwamo madiwani wachache, hawatadhoofika na wataendelea kufanya Kazi.

Sumaye amesema kwamba  wanataka kujenga upinzani  wa kweli wenye lengo la kusaidia wananchi.

Amesema katika kulihakikisha hilo hadi kufikia mwaka 2018 hakutakuwa na kijiji, mtaa utakaokuwa hauna tawi la Chadema.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top