MADIWANI watatu wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) jimbo la Iringa mjini wamemwandikia barua msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa mjini kujiuzulu nafasi zao kuanzia leo Augosti 23 majira ya saa40 jioni
Wakizungumzia azma hiyo ya kujiuzulu nafasi zao madiwani hao Baraka Kimata wa kata ya Kitwiru na madiwani wenzake wawili wa viti maalum Leah Mlelewa na Husna Ngasi walisema kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kuchoshwa na mwenendo wa chama hicho jimbo la Iringa mjini na hivyo wameamua kuachia nafasi zao na kubaki bila kuwa wanachama ama viongozi wa chama hicho.
Kimata ambae alikuwa ni katibu mwenezi wa chadema jimbo la Iringa mjini na mwenyekiti wa madiwani jimbo la Iringa mjini alisema nafasi zake zote ameziacha na kuwa kwa sasa ataendelea na shughuli zake nyingine nje ya siasa kwani siasa kwa ujumla wake imemshinda .
Kwani alisema pamoja na kuwa chama chao ni chama cha Demokrasia ila katika jimbo la Iringa mjini Demokrasia imekuwa ikivurugwa na baadhi ya viongozi na hata kupelekea madiwani kuona chama hichop ni kichungu na hivyo hatua yao ya kujiuzulu ni kilelelezo tosha kuwa ndani ya chama hicho Iringa mjini hakuna usalama.
Alisema mbali ya sababu nyingine zilizopelekea kujiuzulu kwake na wenzake ila bado amekuwa akikosa ushirikiano kutoka kwa mbunge wa jimbo mchungaji Peter Msigwa ambae toka amechaguliwa kata yake hajapata kufanya ziara ya aina yeyote na hivyop kutokana na kubaguliwa huko na pamoja na kuendelea kudidimizwa haki yake wakati wa kuwania nafasi mbali mbali ikiwemo ya umeya na unaibu meya ameona ni vema kutojihusisha na masula la siasa .
" kumekuwepo na maneno kutokana kwa watu kuwa tumenunuliwa kwa ila ukweli utabaki pale pale tumeondoka kwa kukwepa demokrasia mbaya ndani ya chama chetu na tutakuwa huru kujiunga na chama chochote kama ACT Wazalendo ama chama kingine chochote chenye Demokrasia nzuri "
Kwa upande wake Mlelewa ambae alikuwa ni afisa habari wa jimbo la Iringa mjini na katibu wa baraza la vijana la Chadema (BAVICHA ) na katibu wa madiwani alisema ameachia ngazi nafasi zote ikiwemo ya udiwani kama wenzake na sababu za kufanya hivyo ni ubabe ndani ya chama hicho .
Husna Ngasi alisema pamoja na sababu nyingine ameachia ngazi kutokana na kubaguliwa kwa misingi ya itikadi zake za dini na kuwa kwa muda amekuwa akinyanyapaliwa na hivyo kuamua kukaa pembeni .
Kwa upande wake msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa mjini Dkt Wiliam Mfere alipoulizwa na mwandishi wa matukiodaimaBlog kwa njia ya simu jana jioni alisema kuwa bado hajapokea barua ya kujiuzulu kwao kwani hakuwepo ofisini na kuwa akipatatazitolea maelezo
Post a Comment