Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Gwajima kuja na dude hili

Mchungaji Gwajima

Baaada ya kimya cha muda mrefu Askofu Mkuu wa kanisa la ufufuo na uzima, Mchungaji Josephat Gwajima ameibuka na kutangaza kuleta ndege aina ya 'Jet' Tanzania kwa ajili ya kutoa huduma kwa watumishi wake.

Mchungaji Gwajima ambaye hivi sasa yupo mjini Birmingham, Alabama nchini Marekani kwa shughuli zake za injili na mikutano mbalimbali ameahidi ataleta ndege aina ya 'Jet'
"Muda si mrefu nitaleta Tanzania ndege hii 'Jet' kwa lengo la kukuza falme ya Mungu" alisema Gwajima

Mbali na hilo Mchungaji Gwajima akiwa katika ziara zake hizo za kiroho alidai kuwa amepata umeme megawati 250 kutoka nchini Ujerumani ambazo anaamini zitasaidia taifa letu la Tanzania katika kukuza sekta ya viwanda.

"Nimepata Umeme Megawati 250 kutoka Ujerumani kwa ajili ya Taifa letu katika juhudi za kuunga mkono Tanzania ya Viwanda. Nilimtuma Engineer Mkuu wa Ufufuo na Uzima Duniani Eng.Yeconia Bihagaze huko Ujerumani kufanya ufuatiliaji, Umeme huu ni kwa ajili ya Watanzania wote na ujenzi wa uchumi imara wa Tanzania ya Viwanda" alisema Mchungaji Gwajima

Hata hivyo mchungaji Gwajima aliwahi kuahidi pia ataleta treni la kisasa linalotumia Umeme Tanzania.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top