Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkojo wa Masogange ni balaa tupu

Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima, ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa sampuli ya mkojo wa msanii Agnes Gerald maarufu kama Deal ama Masogange (28) umebainika kuwa na dawa ya kulevya aina ya heroin.

Akitoa ushahidi leo Jumatano mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, shahidi huyo wa kwanza wa upande wa mashtaka, akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, ameiambia mahakama kuwa mnamo February 15, 2017 askari wawili kutoka Jeshi la Polisi Tanzania, Koplo Sospeter na WP Judith, walimfikisha Masogange ofisini kwake kwa lengo la kumfanyia vipimo vya mjono wake.

Alisema baada ya kuwapokea, alimsajili Masogange na kumpa namba ya maabara 446 /2017 na kisha kuwakabidhi kifaa maalum kwa ajili ya kuweka sampuli ya mkojo.

Alidai baada ya kupokea sampuli ya mkojo ya Masogange alifanyiwa uchunguzi kwa kutumia kemikali na kubaini kuwa mkojo wake una chembechembe za dawa za kulevya aina ya heroin ambazo kwa kitaalamu zinajulikana kama Diacety Imophine.

Aidha, alisema uchunguzi zaidi ulibaini chembechembe za dawa nyingine ya kulevya aina ya Oxazepam.

Shahidi huyo alidai baada ya kufanya uchunguzi huo, aliandaa taarifa ya uchunguzi kuhusiana na sampuli hiyo ya mkojo ambapo aliisaini yeye mwenyewe na kuthibitishwa na kaimu mkemia mkuu wa serikali.

Shahidi huyo alimtambua Masogange kwa ndiye aliyepelekwa kuchukuliwa sampuli hiyo ya mkojo ofisini kwake.

Pia alidai anaweza kuitambua taarifa hiyo ya uchunguzi kutokana na kuwepo kwa saini yake, muhuri wa moto wa maabara ya mkemia mkuu wa serikali. Pia ameomba mahakama kupokea vitu hivyo kama kielelezo cha ushahidi katika kesi hiyo.
Hata hivyo, mawakili Nehemiah Nkoko na Reuben Simwanza ambao wanamtetea Masogange wamepinga taarifa hiyo ya uchunguzi wakitaka isipokelewe na mahakama kwa madai haijakidhi vigezo vya sheria.

Nkoko amedai utaratibu wa kisheria haukufatwa kabla ya mtuhumiwa aliyeko chini ya polisi kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu, kwa kuwa ofisa wa polisi alitakiwa kuwasilisha maombi mahakamani ndipo amri ya kupimwa itolewe.

Amesema katika ushahidi wake mkemia huyo hajaeleza kama ofisa wa polisi alipeleka amri ya mahakama kutoka mahakama yoyote ile.

"Ripoti ipo kinyume na sheria, mahakama ina njia moja tu nayo ni kuikataa na sio kuikubali. Sheria ipo wazi, tunaomba mahakama ikubali pingamizi letu na kukataa kupokea taarifa hiyo," alisema.

Naye Wakili Simwanza alidai ripoti hiyo ikitazamwa inataja fomu nyingine ya ombi la Jeshi la Polisi kwenda kwa Mkemia Mkuu kwa ajili ya kufanya vipimo.

Amedai ripoti hiyo ipo yenyewe bila ya kuambatanishwa na fomu maalum inayotumiwa na polisi kupeleka sampuli hivyo haiwezi kupokelewa na kutumika kama kielelezo.

Akijibu hoja hizo, Wakili Kakula alidai mapingamizi hayo hayana mashiko wala miguu ya kusimamia.

Amedai fomu ambayo haijaambatanishwa na ile ya mkemia mkuu ni vitu viwili tofauti na hata uwasilishwaji wake unafanywa na watu wawili tofauti.

Alisema taarifa ya mkemia inawasilishwa na mkemia na ile ya polisi inawasilishwa na polisi.

Kuhusu hoja ya sampuli ya mkojo, Kakula alidai kifungu cha 63 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), kimeweka mazingira ambayo ofisa wa polisi atawasilisha maombi mahakamani kuweza kuchukua sampuli.

Alisema iwapo mtuhumiwa anakataa kuchukuliwa sampuli ya mkojo, hivyo atawasilisha ombi mahakamani ili iweze kutolewa amri.

Kakula alisema katika pingamizi lao upande wa utetezi haijaeleza kwamba mshitakiwa alikataa kupima, akalazimishwa. Aliomba mapingamizi hayo yatupiliwe mbali.

Hakimu Mashauri ameahirisha shauri hilo hadi Agosti 28, 2017 kwa ajili ya kutoa uamuzi wa ama kupokelewa kwa taarifa hiyo ama la.

Masogange amefikishwa mahakamani hapo akidaiwa kutumia dawa za kulevya aina ya heroin kati ya Februari 7 na 14, mwaka huu, katika maeneo yasiyojulikana ndani ya jijini a Dar es Salaam.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top