Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NEC yateuwa Madiwani 12 wanawake wa viti maalum

Kwa Mujibu wa Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika kikao chake cha kawaida kilichofanyika  tarehe 21 Agosti, 2017 na baada ya kushauriana na Vyama vya Siasa imewateua Madiwani Wanawake wa Viti Maalum kumi na wawili (12) kujaza nafasi wazi za Madiwani katika Halmashauri mbalimbali Tanzania Bara.
 
Madiwani Wanawake wa Viti Maalumu walioteuliwa ni kama ifuatavyo:

NA.JINACHAMAHALMASHAURI
  1. 1
Ndugu Saida Idrisa KiliulaCUFHalmashauri ya Wilaya ya Kilwa

Ndugu Sophia Charokiwa MsangiCCMHalmashauri ya Wilaya ya Mwanga

Ndugu Shahara Selemani NduvaruvaCCMHalmashauri ya Wilaya ya Mbarali

Ndugu Neema K. NyangaliloCCMHalmashauri ya Manispaa ya Ilala

Ndugu Farida Zaharani MohamedCCMHalmashauri ya Wilaya ya Mvomero

Ndugu Lucia Silanda KadimuCCMHalmashauri ya Wilaya ya Tabora (Uyui)

Ndugu Amina Ramshi MbairaCCMHalmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu

Ndugu Janeth John KaayaCHADEMAHalmashauri ya Wilaya ya Meru

Ndugu Sara Abdallah KatangaCHADEMAHalmashauri ya Manispaa ya Ilala

Ndugu Ikunda MassaweCHADEMAHalmashauri ya Wilaya ya Hai

Ndugu Tumaini Wilson MasakiCHADEMAHalmashauri ya Wilaya ya Siha

Ndugu Elizaberth Andrea BayyoCHADEMAHalmashauri ya Mji wa Mbulu

Uteuzi huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 alitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi uwepo wa nafasi hizo wazi.
 
Imetolewa  tarehe 21 Agosti, 2017
Kailima, R. K
 
MKURUGENZI WA UCHAGUZI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top