Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Panya wamuhamisha Rais Ikulu

Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari, atalazimika kufanyia kazi zake akiwa nyumbani baada ya panya kuharibu ofisi yake iliyopo Ikulu.

Msemaji wa Rais Buhari, Garba Shehu, amesema, panya hao wameharibu samani za viyoyozi katika ofisi hiyo hivyo kiongozi huyo hawezi kufanya kazi katika ofisi mbovu ambayo itakarabatiwa kwa kipindi cha miezi mitatu.

Bw. Garba amesema, hatua ya Rais Buhari kufanyia kazi zake nyumbani hakutaathiri ufanisi wake kwa aina yoyote ile.

Rais Buhari alirejea nyumbani Nigeria Jumamosi iliyopita baada ya kukaa Jijini London nchini Uingereza kwa zaidi ya siku 100 alikokuwa akipatiwa matibabu kwa ugonjwa ambao hata hivyo haujawekwa wazi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top