Baba wa Taifa letu,
Hayati Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kuja na ujenzi wa falsafa yake kuhusu
dhana ya maendeleo. Kwa kutumia hekima, busara na kwa kinywa chake mwenyewe,
Mwalimu Nyerere alisema “ili tuendelee tunahitaji vitu vinne ambavyo ni ardhi,
watu, siasa safi na uongozi bora”
.
Tatizo linalotukumba ni uwepo wa laana inayotumaliza kutokana na kuiasi falsafa ya Baba yetu, Mwalimu Nyerere kwa kupuuzia dhana ya uwepo wa siasa safi na uongozi bora. Hatuwezi kuendelea kwa kuendesha ushabiki upofu ama siasa za maji taka, yaani siasa chafu za kuchafuana na kupakana matope kila kukicha.
.
Tatizo linalotukumba ni uwepo wa laana inayotumaliza kutokana na kuiasi falsafa ya Baba yetu, Mwalimu Nyerere kwa kupuuzia dhana ya uwepo wa siasa safi na uongozi bora. Hatuwezi kuendelea kwa kuendesha ushabiki upofu ama siasa za maji taka, yaani siasa chafu za kuchafuana na kupakana matope kila kukicha.
Mbaya zaidi ni hayo madudu yamekuwa yakifanyika
chini ya mwamvuli “unafki”. Kwa tafsiri ya haraka haraka
neno unafki unaweza ukasema ni undumila kuwili
wa kujivika sura mbili tofauti kwa nyakati moja lakini kwa mahali tofauti
tofauti kulingana na muktadha husika. Lengo kuu la kufanya hivyo ni kutaka
kuharibu uhalisia kwa njia ya mficho na wakati huo huo mtu huyo huyo aonekane
mwema machoni.
Hali hii ya baadhi ya watu kuwa wanafki
haikuanza leo wala jana. Historia inatudhihirishia hilo kuwa hali ya baadhi ya
watu kuutumia mwamvuli huu wa unafki na kuamua
kuwa wanafki, haikuanza leo, wala jana kwani ulikuwapo tangu enzi za utawala wa
kwanza wa Mwalimu Nyerere hadi hii leo katika utawala wa awamu ya nne yake Dk.
Kikwete na utaendelea kuwepo. Utofauti wa unafki upo
kwenye ukomavu wake.
Tuweke kumbukumbu zetu sawa. Mwalimu Julius Nyerere
wakati akiwa madarakani alimwagiwa lawama na tuhuma lukuki kwani wapo waliosema
Mwalimu haambiliki na wengine wakadai anaendesha nchi kwa “remote” akiwa
Butiama (kijijini kwao). Lakini mara baada ya kung’atuka kwa hiari Urais ndipo
sifa za kinafki zilianza kummiminikia huku tukianza kumuita “Baba wa Taifa”. Mara baada umauti kumkuta ndipo unafki ulizidi
kwake na leo hii kila kitu kibaya kinachotokea tunasema laiti Mwalimu Nyerere
angekuwepo haya yote yasingetokea. Lakini angali hai ama madarakani
hatukuyatambua haya zaidi ya kuuendekekeza unafki.
Ama Alhaji Hassan Mwinyi wakati akiwa Rais wa awamu ya
pili walimwita mbinafsi, muuzaji nchi kutokana na ubinafsishaji lakini leo hii
ni mstaafu wanaanza kummwagia sifa teletele na hata kumwita “Mzee
wetu” huku wakijivunia kuchota hekima na busara kutoka kwake lakini angali
madarakani hatukuliona hilo. Huu ni unafki mtupu.
Pia Benjamini Mkapa alidhihakiwa kweli kweli
wakati wa uongozi wake hadi kufikia hatua ya kumwita ‘ukapa’ badala ya Mkapa
kutoka katika neno la ‘ukata’. Lakini leo hii kila anapokatiza ni shangwe,
makofi, vifijo, na vigelegele na tukisema afadhali ya Mkapa kuliko wote na
wengineo tumewaona wakimpa hata tuzo ya heshima. Jamani! Kama huu si unafki, basi tuuiteje?
Hata Dk. Jakaya Kikwete (JK) alipokuwa madarakani
walimuita majina mengi ya hovyo hovyo. Wapo waliomuita “Mzee wa kutabasamu”,
Serikali yake ni dhaifa na legelege! Lakini hekima na busara kubwa aliyojaaliwa
Dk. Kikwete hakuweza kuwajibu lolote waliokuwa wakimkejeli na badala yake
aliwaambia mtanikumbuka.
Kikwete alisema: “Mtaumbuka baada ya 2015”. Dk. Kikwete
aliwaambia wanaombeza sasa wataona aibu baada ya kumaliza kipindi chake. Naam!
Ni kweli Watu waliokuwa wakimbeza wameanza kuumbuka na kunza kupayuka hadharani
kuwa wana mkumbuka.
Wale waliokuwa wakidai JK ni legelege na dhaifu wanataka
Rais mkali ndio hao hao leo hii wanasema Rais Magufuli ni dikteta; Wale
waliokuwa wanasema JK hawezi kuchukua maamuzi magumu ya kutimua wanaoharibu,
ndio hao hao leo hii wanaosema kuwatumbua “kuwafukuza” wanaoharibu ni kinyume na haki za binadamu;
Mara JK hakamati mafisadi Papa ama hawakamati wauzaji madawa ya kukevya, leo
hii wameanza kukamatwa wanaanza kuwatetea kwa kusema si vyema kuwataja watu
majina, mara si vyema kuwakamata waliolitumikia Taifa letu!
Ajabu na kweli ni kuibuka kwa Mwenyekiti wa Chadema
Taifa, Freeman Mbowe kusema hali ya kimaisha wakati wa utawala wa Kikwete
ilikuwa bor zaidi. “Maisha yalikuwa safi enzi za Kikwete” amesema Mbowe.
Mbowe ameanza kujivua nguo kwa kutaka leo hii
kuwaaminisha Watanzania kwamba maisha yalikuwa mazuri kipindi cha JK kuliko
kipindi hiki cha JPM. Kibaya zaidi hajaja na utafiti wa kitaalamu kuthibitisha
kauli yake bali kaamua kujisemea tu ilimradi asikike kuwa anasema.
Kama kweli maisha yalikuwa mazuri kwanini walikuwa
wakimkashifu mtu (JK) ambaye amewanyooshea Watanzania maisha yao? Kulikuwa kuna
sababu gani kwa Mbowe na kundi lake kumfedhehesha majukwaani kwamba Serikali
yake ilikuwa dhaifu na maisha yalikuwa magumu? Leo hii wanamponda Rais
Magufuli, kwanini tusiamini kwamba akitoka madarakani nae wataanza kumsifia?
Jana wakati Kikwete yupo madarakani walisema maisha
magumu, leo hii hayupo madarakani wanamsifu kuwa maisha yalikuwa bora! Huu ndio
unafki wenyewe unaofanywa na Wanasiasa usio na tija kwa umma.
Bila shaka haya marashi ya kinafki yalioanza kupulizwa
tangu enzi za utawala wa awamu ya kwanza hautaiacha awamu hii ya tano. Leo hii
Rais Magufuli anatukanwa vibaya mno kwani kila mtu anayejisikia kumuongea
vibaya anafanya hivyo. Lakini subiria akitoka madarakani, hizo sifa atakazo
mwagiwa, usizipimie kabisa!. Rais Magufuli awe sawa kimkao na marashi haya ya
kinafki.
Unafki niliouzungumzia
ni sehemu ya khulka ya kawaida kabisa kwa asilimia kubwa ya watu kutokupenda
kuzungumzia mazuri ya mtu akiwa hai wanasubiria mpaka awe amefariki ndipo wamzungumzie
kwa mema; Ama wale walio katika uongozi huwa hawasifiwi kwa kile wanachokifanya
mpaka wamalize muda wao wa uongozi ndipo sifa kedekede huanza kumiminika. Yote
hayo ni sehemu ya unafki wetu sie tusio na
shukrani.
Hivi watapungukiwa na kitu gani endapo watamsifia Rais
Magufuli kwa utekelezaji wa ilani anaoufanya? Watapungukiwa na nini wakimsifia
kuwa anatoa elimu bure, amenunua ndege 4 mpya, anajenga reli ya kisasa, anafuta
kodi kero kwenye kilimo, anapeleka umeme vijijini, anapeleka maji vijijini!
Watapungukiwa nini wakimsifia? Watapungukiwa nini wakisema ukweli amepunguza
kasi ya kiwango cha rushwa na kurejesha nidhamu ya uwajibikaji kwa Watumishi wa
umma. Kwanini hawajifunzi kuusema ukweli wa hali ilivyo?
Baadhi ya Watanzania wanashindwa kuunga mkono ama kutoa
ushirikiano wa kutosha kwa juhudi zinazofanywa na Serikali kwa sababu tu wapo
Watu wachache ambao kazi yao kuupindisha ukweli, kazi yao kuhakikisha
wanarudisha nyuma maendeleo kwa maslahi yao binafsi na si ya kitaifa. Kuna haja
ya kuanza kutokufuata mkumbo wa kuamini kila lisemwalo nao kuwa ni sahihi kwani
mara baada ya mtu kutoka madarakani huanza kumsifia wakati hapo awali walikuwa
wakimponda.
Hila, roho mbaya, tamaa za fisi za uchu wa madaraka na
mali huwafikisha kwenye upindishaji wa mambo kwa maksudi ilimradi ukweli
uonekane ni uongo, kwa kuwaamisha watu uongo wao pasipo kujua kuwa umma
wanaujua uongo wao.
Ipo mifano mingi tu ya kuelezea jinsi gani unafki unaofanywa, unavyotuletea umaskini. Unafiki umezaa
kitendo cha kupuuzia falsafa ya Mwalimu Nyerere kwa kudharau dhana ya uwepo wa
siasa safi na uongozi bora ambayo alituasa tuyazingatie.
Laiti kama unafki ungelikuwa
ni pesa, basi watu wangekuwa matajiri. Kwani leo hii baadhi ya watu wameigeuza
nchi hii kuwa kama Taifa la Makambare. Si
Mtoto, Mama wala Baba wote ni wanafiki watupu. Tuukatae unafki huu!
1 comments:
Unafiki ni mbaya na Wahenga waliisha sema,"Msemakweli ni mpenzi wa Mungu"!
ReplyWabariki Mungu anawaona!
Ya Mbowe na Kampuni yake:CHADEMA iliyokodiwa na Bilionea Lowassa hatuyashangai kuwa na "ndimi-mbili", jana wakituaminisha pale MwembeYanga wanao ushahidi Lowassa FISADI #9, na leo hii ni Kamanda, akigombea na Urais!
Unafiki utawaadhibu kwenye Sanduku la Kura!
Post a Comment