Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Waziri Nchemba Atishia Kuwafutia Uraia Watanzania Wabaguzi

Waziri wa mambo ya ndani Mh. Mwigulu Nchemba ametishia kuwafutia uraia watanzania wapya wa Katumba mkoani Katavi ambao walikuwa wakimbizi kwa muda mrefu kutokana na tabia ya ya baadhi yakubaguana kitaifa na kikanda.

Waziri Nchemba amesema hayo jana  wakati  alipopita kwenye kambi kuangalia usajili unaendeleaje ambapo amesema  wananchi   hao waliopewa uraia wakitokea burundi wakati wa vita ya kikabila miaka 1972 wamekuwa na tabia ya ubaguzi hata kufikia kushindwa kusaidiana kwenye biashara zao.

Waziri aliwaambia wananchi hao kuwa yeyote atakayeleta mambo ya ubaguzi ikiwa ni pamoja na kubaguana kibiashara  katika jamii hatosita kumfutia uraia alioupata kwani Watanzania hawana mambo ya kibaguzi.

Pamoja na hayo Kiongozi huyo alitumia muda huo kuwataka Watanzania kuwa na utanzania ndani ya mioyo yao na waache tabia ya kutaka kukwamisha kila kitu kinachofanywa na serikali kwa kuweka vikwazo mbele ili vitu visifanikiwe.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top