Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Magufuli awasili SALAMA Nchini Uganda

Rais John Magufuli leo amewasili nchini Uganda, kuhudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaofanyika  mjini Kampala.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Entebbe, Rais Magufuli amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Sam Kutesa na kisha kuelekea Ikulu ya Entebbe.

Baada ya kuwasili Ikulu amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Uganda  Yoweri  Museveni.

Pia kesho atahudhuria mkutano maalum katika ngazi ya wakuu wa nchi unaohusu masuala ya miundombinu na afya na keshokutwa atahudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top