Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wazalisha Dawa Kutoka Nchi 130 Wakutana Na Bohari Ya Dawa (MSD) Jijini Dar Es Salaam

Na Dotto Mwaibale
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt.Mpoki Ulisubisya, amesema uwezo wa Bohari ya Dawa (MSD), umeongeza na kupanua wigo wa uwekazaji na uzalishaji wa dawa nchini.

Akizungumza kwenye Mkutano wa pili wa mwaka wa MSD na wazalishaji na washitiri wa dawa na vifaa tiba zaidi ya 130 kutoka nchi 25, Dkt. Mpoki amesisitiza kuwa, MSD niya kiwango cha kimataifa hivyo milango iko wazi kwa wawekezaji wa dawa na vifaa tiba kuja kuwekeza nchini.

Aliongeza kuwa mkutano huo ni fursa ya kubadilishana uzoefu na kujadili namna yakufanya manunuzi,utekelezaji wamikataba na uimarishaji wa uwekezaji katika sekta ya afya.

“Tunaitikia wito wa serikali wa kuhakikisha wawekezaji wa ndani wanapewa kipaumbele, hivyo mkutano huu wakiutendaji,utaijengea uwezo MSD na kuongeza ushirikiano kati yake na wawekezaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba kwa kujua mahitaji aliyopo na kuwashauri soko tulilonalo ndani na njeya nchi ilikupanua wigo wautendaji,”alisema.

Aidha alisisitiza  kuwa  uwezo wa MSD katika usambazaji wa dawa na vifaa tiba umekua na  ndio sababu ya kukidhi viwango vya kimataifa, huku  mwaka wa fedha uliopita wakiwa wameweza  kutumia dola milioni 700 kwa ajili ya kufanya manunuzi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole Gabriel, alisema utendaji wa MSD meboresha huduma za afya nchini na uhusiano wa karibu kati ya wizara yake na sekta ya afya nikichocheo muhimu cha uchumi nchini.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Rugambwa Bwanakunu, alisema hatua ya bohari kununua dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji, imewawezesha kupanua wigo wa huduma na  kuwa karibu na wafanyabiashara na wawekezaji 160 alioingia nao mikataba, hivyo mkutano huo utawajengea uwezo na kuongeza ushindani kwa wazalishajihao.

Aidha, kwa upande wake mwakilishi wa wazalishaji wa ndani, kutoka kiwanda cha Prince Phermaceutical,HetalVitalan, lisema uimarishaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba  hapa nchini,umesaidia fedha inayotengwa na serikali katika bajeti ya dawa  kuweza kukuza uchumi wa ndani,kuongeza ajira kwa watanzania  na kupanua wigo waukusanyaji wa kodi kwa viwanda vya ndani.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top