Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wabunge waliokwepa safari watakiwa kurejesha posho

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.PICHA|MAKTABA 
********
Sakata la wabunge waliochukua posho kwa ajili ya safari za mafunzo nje ya nchi na kuacha kusafiri, limeingia hatua mpya baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuwataka wazirudishe.
Katika orodha ya wabunge wanaotajwa katika sakata hilo, wamo baadhi ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha NCCR-Mageuzi.

Sakata hilo liliibuliwa bungeni wiki iliyopita mjini Dodoma na Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy (CCM) wakati akichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (Laac).
Keissy alisema baadhi ya wabunge wanapaswa kuchunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa kuchukua posho za safari za nje ya nchi lakini hawakwenda safari hizo.
Mbunge huyo alifafanua kuwa mbali na kutokwenda kabisa safari hizo, lakini wapo ambao walikwenda na hawakukaa siku zote zilizopangwa.
“Tunawajua na wapo humu ndani,” alisema huku baadhi ya wabunge wakipaza sauti wakitaka awataje, lakini yeye akasema siyo jukumu lake kuwataja kwani Ofisi ya Bunge inawajibika kufanya hivyo.
Mbunge huyo alienda mbali na kudai mbunge mmoja alikatisha safari ya kwenda Marekani na kuamua kwenda Dubai kwa safari binafsi ambayo haikuwepo katika ratiba ya ziara hiyo ya mafunzo.
Habari za uhakika zilizopatikana jana zilisema wabunge wanane walichukua posho ya safari ya kati ya Sh5 milioni na Sh6 na Spika amewaandikia barua akiwataka warudishe fedha hizo.
Majina ya wabunge hao tunayo, lakini kwa sababu za maadili ya uandishi wa habari, gazeti hili halitaweza kuwataja kwa kuwa hawakupatikana ili kujibu tuhuma hizo kama maadili yanavyoelekeza.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake bungeni mjini Dodoma jana, Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alisema kuwa Spika ameshaliona jambo hilo na kulichukulia hatua za kiutawala.
“Spika amewaandikia barua akiwataka kurejesha fedha zote za safari ambazo hawakwenda. Ni lazima wazirudishe hakuna namna,” alisema Joel ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Shughuli za Bunge.
Alipoulizwa kuhusiana na majina yao na kiasi walichochukua, Joel alisema hilo ni jambo la kiutawala na kwamba Spika ndiyehuarifiwa na kamati kuhusiana na wabunge ambao hawakusafiri.
 
MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top