Loading...
CCM yakunjua makucha yake
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekunjua makucha kwa kuwachukulia hatua kali za kinidhamu kwa viongozi na wanachama wake 600, waliobainika kukiuka maadili ya uongozi, ikiwemo kukisaliti Chama katika kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita.
Wanachama hao ni kutoka katika mikoa 10 ya Tanzania Bara, ambayo imeshawasilisha ripoti zake makao makuu ya CCM, kuhusu hatua iliyochukua dhidi ya wanachama waliokisaliti wakati wa uchaguzi huo.
Katika orodha hiyo, wapo wanachama waliopewa onyo kali, waliosimamishwa uongozi na wengine kuvuliwa uanachama. Pia wapo wanaosubiri maamuzi ya vikao vya juu kutokana na tuhuma zinazowakabili.
Post a Comment